Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Wednesday, January 27, 2016

ZUBERI ZITTO KABWE:AITAKA SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WABADHIRIFU WA TSHS BIL. 28 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA TABORA



 
ZUBERI ZITTO KABWE
Na Paul Christian.

Mbunge wa Kigoma mjini Zuberi Zitto Kabwe ameihoji serikali ni lini itawakamata na kuwafikisha mahakamani wabadhirifu wa shilingi bilioni 28 za wakulima wa Tumbaku mkoani Tabora uliofanywa na viongozi wa Chama Kikuu Cha Ushirika wa wakulima wa Tumbaku kanda ya Magharibi WETCU na wengine.

Kabwe ametoa hoja hiyo leo bungeni mjini Dodoma wakati akiuliza swali la nyongeza ambapo amesema  mwaka 2013 Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali CAG alitoa taarifa ya upotevu wa fedha za wakulima wa Tumbaku wa mkoa wa Tabora.

Ameongeza kuwa, "aliyekuwa Rais katika serikali ya awamu ya Nne alikwenda Tabora na kuagiza viongozi wa WETCU na wahusika wote wa ubadhirifu ule wakamatwe mara moja na kufikishwa mahakamani lakini mpaka leo hii hakuna ambaye amekamatwa wala kufikishwa mahakamani."

Kabwe amesema, "wakulima kupitia vyama vyao vya msingi inabidi walipe fedha zile bilioni 28, serikali ya awamu ya Tano inachukua hatua gani dhidi ya watu hawa ambao wamewaibia wakulima wa Tumbaku na kuwafanya waendelee kuwa masikini licha ya kwamba wanajitahidi kulima mwaka hadi mwaka."

Akijibu swali hilo la nyongeza Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mwigilu Nchemba amesema, “mheshimiwa spika hivi tunavyoongea tayari ninayo hiyo ripoti ya Mkaguzi na ninaipitia mstari kwa mstari na ninategemea baada ya bunge hili nitapitia katika maeneo hayo yanayolima tumbaku hasa hasa mkoa wa Tabora kwa ajili ya kwenda kufuatilia utekelezaji wa maagizo ya mheshimiwa Rais aliyoyatoa."


No comments: