Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Thursday, January 14, 2016

MAJI YA BWAWA LA IGOMBE KUSHINDWA KUTOSHELEZA MAHITAJI IFIKAPO 2019

MKURUGENZI MTENDAJI WA TUWASA INJINIA MKAMA BWIRE AKIWASILISHA MADA YA UPATIKANAJI WA MAJI KATIKA MANISPAA YA TABORA MBELE YA MADIWANI WA MANISPAA HIYO

Na Paul Chriatian, Tabora.

Imeelezwa kuwa maji ya bwawa la Igombe yanayohudumia wakazi wa Manispaa ya Tabora hayotoweza kutosheleza mahitaji ya watu wa Manispaa hiyo ifikapo mwaka 2019.

Akiwasilisha mada ya hali ya upatikanaji maji katika Manispaa hiyo Mkurugenzi mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira TUWASA injinia Mkama Bwire amesema upungufu huo wa maji utatokana na ongezeko la idadi ya watu.

Amasema mamlaka hiyo kwa sasa inazalisha maji ya lita za ujazo milioni 15 kwa siku, huku mahitaji halisi kwa wakazi wa Manispaa hiyo ambao ni zaidi ya 250,000 ni lita za ujazo milioni 24.005 kwa siku.

Mkurugenzi huyo ameeleza kuwa lita hizo za ujazo milioni 15 zinazozalishwa na mamlaka hiyo zinahudumia kata 19 kati ya kata 29 za Manispaa hiyo, huku lengo likiwa kuzifikia kata zote.

Injinia Bwire amesema Mamlaka hiyo itakuwa na uwezo wa kuzalisha maji ya lita za ujazo milioni 30 kwa siku ifikapo mwezi Machi mwaka huu na hivyo kuondoa  mgawo wa maji uliopo hivi sasa, baada ya kukamilika ujenzi wa machujio mapya na kukarabati ya zamani.

Mkurugenzi huyo wa TUWASA amesema ili kukabiliana na hali hiyo ya bwawa la Igombe kufikia ukomo wake kutosheleza mahitaji ya wakazi wa Manispaa ya Tabora miradi ya maji kutoka ziwa Victoria na mto Malagarasi ni muhimu kutekelezwa.

Injinia Bwire amebainisha kuwa mradi wa maji ya ziwa Victoria umefikia hatua ya wizara ya husika kutangaza zabuni mwishoni mwa mwaka jana ili apatikane mkandarasi wa kuifanya kazi hiyo ya kutoa maji katika kijiji cha Solwa kilichpo Shinyanga vijijini.

Aidha amesema mradi huo utatekelezwa na wakandarasi tofauti ambao watagawana kutoka Shinyanga-Nzega, Nzega-Tabora na Nzega Igunga na kwamba utagharimu shilingi bilioni 279,390,444,272.19
 
Semina hiyo ya hali ya maji katika Manispaa hiyo imeandaliwa na TUWASA ikiwalenga madiwani wa Manispaa hiyo kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kuendeleza huduma muhimu ya maji kwa wakazi wake.


No comments: