Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Friday, January 8, 2016

HALMASHAURI YAAGIZWA KUMZAWADIA DEREVA ALIYETUMIA FEDHA ZAKE KUFANYA KAZI YA UMMA



 
MBUNGE WA JIMBO LA ULYANKULU JOHN KADUTU AKIMPONGEZA DEREVA ADREY

Na Paul Christian, Tabora

Mbunge wa Jimbo la Ulyankulu John Peter Kadutu ameiagiza halmashauri ya wilaya ya Kaliua mkoani Tabora kumzawadia dereva wa gari la wagonjwa (ambulance) la kituo cha afya cha Ulyankulu kufuatia kujitolea kwa fedha zake za mfukoni kutengeneza kitanda cha kubebea wagonjwa kwenye gari hilo ambacho hakikuwepo.
KITANDA KILICHOTENGENEZWA KWA FEDHA ZA DEREVA ADREY

Amesema mtumishi huyo Adrey ameonesha moyo wa kizalendo na ari ya kipekee inayofaa kuigwa na watumishi wengine katika jimbo hilo na kwamba anastahili kuenziwa rasmi kwa kitendo hicho. 


Agizo hilo limetolewa mbele ya mwenyekiti wa halmashauri hiyo Haruna Kasele,mwenyekiti wa kamati ya elimu, afya na maji ambaye pia ni diwani wa kata ya Uyowa Alphonce Msanzya na mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo afisa utamaduni na michezo Marko Kapela.
 

No comments: