Kiongozi
wa kambi ya upinzani bungeni Freeman Mbowe ameitaka serikali kutoa kauli kuhusu
katazo la mikutano ya vyama vya siasa mara baada ya uchaguzi mkuu, Shirika la
Utangazaji la Taifa TBC kusitisha matangazo ya moja kwa moja ya Bunge na
matumizi ya majeshi Zanzibar na kwingineko.
Mbowe
amesema hayo leo Bungeni mjini Dodoma wakati wa kipindi cha Maswali ya papo kwa
papo kwa Waziri mkuu.
Kiongozi
huyo wa kambi ya upinzani Bungeni amesema, “mheshimiwa Waziri mkuu ukiwa
kiongozi wa shughuli za serikali Bungeni na wewe ukiwa kama mwanasiasa mzoefu
ninahakika unatambua kwamba ujenzi wa demokrasia ni gharama na mchakato wa muda
mrefu na nina hakika utakuwa unajua vile vile kwamba nchi yetu imepiga hatua
katika kujenga jamii inayoheshimu demokrasia, inayoheshimu sheria na inaheshimu
katiba ya nchi.”
Ameongeza,
“katika muda mfupi tangu serikali ya awamu ya tano imeingia madarakani yapo
mambo matano makubwa yaliyotokea ambayo yanahashiria aidha serikali hiyo haiheshimu
kukua kwa demokrasia katika taifa ama pengine inadhamira ya kuondoa lengo kubwa
hilo lililowekwa na Katiba ya taifa.”
Mbowe
katika kujenga hoja ya swali lake amesema, “Mheshimiwa Waziri mkuu baada ya
uchaguzi mkuu wa 2015 jeshi la polisi limeweka makatazo nchi nzima kwa vyama
vya siasa kutokufanya kazi zake za siasa, haki ambayo ni ya kikatiba, na leo
tayari ni miezi mitatu na siku tatu,katazo hilo linaendelea na katazo hilo mheshimiwa
waziri mkuu uliliunga mkono na kusisitiza katika mkutano wako ulioufanya katika
jimbo la lako la Ruhangwa kwamba wenye haki ya kufanya ni wale walioshinda
lakini vyama vya siasa haviendelei kuruhusiwa kufanya kazi za siasa.”
Kiongozi
huyo wa kambi ya upinzani Bungeni katika sehemu ya kwanza la swali lake
ameuliza, “mheshimiwa waziri mkuu unataka kulithibitishia bunge hili,nchi hii
na dunia hii kwamba wewe kama kiongozi mkuu wa shughuli za serikali unakusudio
la kuendelea kuzuia vyama vya siasa kufanya shughuli zake za kisiasa ambayo ni
haki yao ya Kikatiba.”
Katika
sehemu ya pili ya swali lake amesema, “mheshimiwa waziri mkuu tukifuatana na
hapo hapo unatambua vile vile kwamba urushaji wa matangazo ya moja kwa moja ni
haki ya kikatiba ya wananchi kupata taarifa na shirika la habari la taifa ni
shirika la umma, lakini ndani ya bunge mheshimiwa waziri mkuu kuna taarifa
zilizorasmi kabisa serikali yako imetoa kauli hapa kuzuia urushaji huo wa
matangazo.”
Mbowe
ameeleza, “Sambamba na uzuiaji huo wa urushaji wa matangazo kumeendelea kuwepo
kwa matumizi makubwa ya majeshi yetu, kuanzia Zanzibar hadi hapa, na Zanzibar
katika kupinga matokeo ya uchaguzi ya Zanzibar ambao ulikuwa uamuzi wa
wananchi, mheshimiwa waziri mkuu unaiambia nini Dunia kwa awamu yako ya Tano
sasa imekubali kuwa utawala wa kijeshi kwa mgongo wa utawala wa Kidemokrasia?”
![]() |
WAZIRI MKUU MAJALIWA K. MAJALIWA |
Akijibu
maswali hayo Waziri mkuu mheshimiwa Majaliwa Kassimu Majaliwa amesema, “Mheshimiwa
Spika, kwanza niseme namshukuru sana kiongozi wa kambi ya upinzani kwa maswali
yake mawili ambayo yanahitaji ufafanuzi na watanzania waweze kujua,kwamba
uongozi huu wa awamu ya Tano ni uongozi unaoongoza kwa kufuata Demokrasia,
kanuni, sheria na taratibu kadiri ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilivyo.”
Waziri
mkuu ameongeza, “yapo mambo yanajitokeza na tunapojaribu kutoa maelekezo ya
kimsingi kuweza kufuatilia na kwa sababu ya utaratibu wa mazoea tu yanaweza
kutafsiriwa vinginevyo suala lako la makatazo ya vyama vya siasa kufanya
mikutano ni jambo ambalo naweza kusema msemaji wa kwanza kabisa hakutumia
nafasi yake ya uandishi kuandika kwa mfululizo kwa sababu ni mimi ndio ambaye
nilikuwa nimefanya ziara kwenye jimbo langu kusalimia wapiga kura wangu.”
Majaliwa
ameendelea kujibu, “mimi ni mbunge kama nyie na ninapokuwa Ruhangwa sivai koti
la waziri mkuu bali nakuwa mbunge nazungumza na watu wangu nimekuwa na vikao
mbalimbali vya makundi mbalimbali nikiwashukuru binafsi kwenye jimbo langu
ambako najua tunautamaduni wetu nimepita pia kwenye kata ambazo pia madiwani
wetu ni wa vyama vya upinzani, lakini tumeweka msimamo wa vyama vyote kwenye
jimbo lile kwamba lazima sasa tufanye kazi za maendeleo kwenye jimbo letu.”
Amefafanua,
“ na kama mwandishi yule angeweza kuweka mtiririko wa ziara zangu na matamko
yetu ndani ya wilaya yangu, kwa jimbo langu, angeweza kunitendea haki, kwa
sababu nilichotamka mimi kilifuatiwa na kauli zilizotamkwa na madiwani kwenye
kata ambako nimetembelea wakiwemo wa upinzani ambao walisisitiza na kutoa msimamo
kwamba sasa jimbo hili tunataka tufanye kazi suala la siasa tunaliweka pembeni.”
Amesema,
“ suala la siasa tunaondoa tofauti zetu, hayo yanazungumzwa na madiwani
wenzangu wa vyama vingine kwa hiyo ni jambo jema wanapolitamka kwa wananchi
wanalitamka kwa wananchi kwa maana ya kuweka msimamo wa maendeleo.”
Waziri
mkuu amefafanua, “mtiririko ule tulizungumza pia na baraza la madiwani, nimezungumza
na wafanyakazi wa halmashauri, nimezungumza na baraza la wazee, nimezungumza na
wakinamama na pia nikazungumza na jeshi
la polisi wale ni sehemu ya raia walioko kwenye jimbo langu, mimi nimefanya
kazi nyingi sana kwao na wao wamefanya kazi nyingi sana kwangu.”
Ameongeza,
“Kwa hiyo kauli yangu ilikuwa inatokana na mazingira yale kama mwandishi
angeamua kufanya kazi zake vizuri kwa kueleza shughuli zangu hata nilipotamka
kwamba kuanzia sasa maeneo tumeamua tufanye kazi tu bila kuzingatia itikadi za
vyama vyetu na kwamba sasa mambo ya siasa tuache pembeni.”
Majaliwa
amefafanua, “Wale wote ambao sasa wangetakiwa kupita kwenye maeneo
yawalioshinda ni wale tu ambao wameshinda kwenye maeneo yao kwa hiyo jambo lile
kama lingekuwa limeelezwa, limeripotiwa kwa mtiririko ule wala lisingeweza
kuleta tafsiri ambayo imekuja kutoweka.”
Amisisitiza,
“mimi najua utawala wa sheria, najua vyama vya siasa vinahaki yake,najua nchi
imeamua na inatambua kwamba chama cha siasa kinaweza kufanya mikutano.”
Amesema,“Lakini
pia kama msingi ule wa kauli ya wanajimbo la Ruhangwa utaweza kufuatwa na watu
wengine unaweza kuwaletea tija pia,kwa kusema hilo niseme tu kwamba jambo lile
lilitokana na mazingira ninamoishi na sikulitamka kama waziri mkuu, nilitamka
kama mbunge wa jimbo na lilitokana na matamko ya sisi wawakilishi wa vyama vya siasa
tuliomo kwenye jimbo lile mheshimiwa spika.
Waziri
mkuu Majaliwa akijibu sehemu ya pili ya swali aliloulizwa amesema, “eneo la
pili ni lile ambalo mheshimiwa umetaka kujua kauli ya serikali juu ya TBC
kuacha kutangaza siku nzima na badala yake watatangaza vipindi vya maswali na
majibu baada ya hapo wataendelea na shughuli zao na huku wakirekodi ili
watutangazie baadae.”
Amesema,
“mheshimiwa waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo amelifafanua vizuri
sana jana kwenye kipindi maalum na ninaamini watanzania wametuelewa, haukuwa na
lengo, TBC haijaacha kutangaza walichofanya ni kubadilisha ratiba, matangazo ya
bunge yataendele kutangazwa lakini tumeondoa muda badala ya ule muda wao
waneweza kufanya matangazo ya kibiashara na matangazo mengine.”
“Suala
la bunge waandishi wao wapo, TBC inawawakilishi Dodoma watafanya rekoding
halafu baadae watatafuta muda mzuri ambao tunaamini watanzania wengi watapata
muda mzuri wakuweza kusikiliza matangazo yao.”Amesema Majaliwa.
Amesema “huo ni mpango wa taasisi yenyewe wa
ndani unaotokana na kazi wanazozifanya wanajua matatizo na faida wanazozipata
ndani ya taasisi kwa hiyo wanapoishauri wizara, wanapoieleza wizara na kwa kuwa
waliisha anza kutekeleza watanzania waliona mkatiko wa matangazo pia kulikuwa
na muongozo ulitolewa hapa kwa hiyo tukasema jambo hili lazima kuwe na kauli ya
serikali kwa watanzania kwa sababu muongozo ulitolewa na mmoja kati ya wabunge
wetu anataka kujua kwa nini kuna mkatiko wa matangazo hivyo ndivyo ambavyo
ilivyokuwa na huo nadhani msimamo wa TBC na ndio msimamo wa serikali.”
Akijibu
kuhusu matumizi ya majeshi waziri mkuu amesema “Mheshimiwa ametaka pia kujua
matumizi ya majeshi, majeshi yetu yapo
kwa malengo kwamba lengo kuu ni kutunza amani na utulivu ndani ya nchi,wajibu
wao mkubwa ni kuhakikisha kwamba watu kwa maana ya watanzania kwa majeshi ya
Tanzania wajibu wake ni kuhakikisha watu wetu wanafanya shughuli zao kwa amani
na utulivu na wako nchi nzima.
Ameongeza
kusema, “jukumu lao ni kumlinda mtanzania popote alipo bila ya kukiuka misingi
ya jambo analolifanya wakati huo, wako pia Zanzibar, wako pia Tanzania Bara na
wote hao kazi yao na jukumu lao ni lile lile sasa wanaweza kulazimika kutumia
nguvu pale ambako wanapoona utaratibu ulioko eneo hilo unakiukwa.”
Majaliwa
amesisitiza, “ na hiyo ndio kazi ya jeshi na polisi kwamba wataendelea kutunza
amani ili watanzania walioko kwenye eneo hilo kila mmoja afanye shughuli yake
kila mahali kunautaratibu wake, kila mahali kuna msingi wake na ningetarajia
eneo hilo, wote walioko kwenye eneo hilo, wanaofanya jambo hilo, wafanye jambo
hilo kwa msingi unaofanana, usiokiuka taratibu za eneo hilo kwa hiyo jeshi la
polisi lipo na litaendelea kufanya kazi yake kwa uaminifu, uadilifu na ninaomba
sana tuwasaidie jeshi la polisi kufanya kazi yao bila ya usumbufu ili
wasionekane wanafanya kazi nje ya utaratibu wao.”
No comments:
Post a Comment