Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Tuesday, January 26, 2016

SUNDAY OLISEH AOMBA RADHI KWA NIGERIA KUTUPWA NJE MICHUANO YA CHAN 2016



 
SUNDAY OLISEH NA WACHEZAJI WA NIGERIA
Na Paul Christian, Tabora.

Timu ya taifa ya Nigeria imeondolewa kwenye mashindano ya ubingwa wa mataifa ya Afrika kwa timu za taifa zinazoundwa na wachezaji wanaocheza ligi za nchi husika CHAN 2016 baada ya kukubali kichapo cha bao 1 kwa bila kutoka kwa Guinea.

Nigeria “Super Eagle” imeondolewa kwa kufikisha pointi 4 nyuma ya vinara wa kundi C Tunisia na Guinea iliyojikusanyia pointi 5 baada ya ushindi wa mechi hiyo ya mwisho ya kundi hilo.

Mchezaji wa Guinea Ibrahima Sankhon ndiye aliyeifungia timu yake ya Guinea bao la pekee kunako dakika ya 45 ya mchezo na kuifungashia virago Super Eagle katika mechi iliyopigwa Jumanne.

Kabla ya mechi za mwisho za kundi hilo Super Eagle inayonolewa na Sunday Oliseh ilikuwa ikiongoza kundi hilo ikiwa na pointi 4.

Mechi nyingine ya kundi hilo ilizikutanisha Tunisia na Niger ambapo Tunisia imeibamiza Niger kwa magoli 5 kwa bila na kuongoza kundi hilo.
Katika kundi hilo Tunisia na Guinea zimevuzu hatua ya robo fainali katika michuano hiyo.

Hata hivyo kocha wa Nigeria Sunday Oliseh amewaomba radhi mashabiki wa Super Eagle na wanageria kwa kutolewa mapema katika michuano hiyo ya CHAN 2016.

Nigeria iliwakilishwa na: Ezenwa, Alimi, Obaroakpo, Akas (C), E. Matthew, Onobi, Matthew, Usman, Aggreh, Adeniji, Okoro

Guinea iliwakilishwa na: 16. Keita (C), 2. Thiam, 5. Bangoura, 6. Sankhon, 8. Soumah, 12. Sylla, 13. A. Camara, 15. Camara A, 17. D. Camara, 19. Youlla, 23. A.L. Camara.

No comments: