Na Hastin Liumba,Uyui
JUMLA ya nyumba 415 zimebomoka na kusombwa na maji kufuatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha wilayani Uyui mkoani Tabora.
Mkuu wa wilaya hiyo Zuhura Ali amesema hayo wakati akitoa taarifa ya serikali kwenye kikao cha baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya hiyo kilichofanyika Isikizya wilayani humo.
Amesema licha ya kaya hizo kuathirika, jumla ya ekari 225
za mazao mbali mbali zimeaharibiwa vibaya na mvua zinaendelea kunyesha wilayani humo.
Mkuu huyo wa wilaya amesema ekari 342 za tumbaku nazo zimaharibiwa vibaya na mvua hizo.
Amebainisha kuwa mvua hizo pia zimeathiri miundombinu ya barabara au kuyafanya maeneo kutofikika kufuatia barabara kufunikwa na maji.
JUMLA ya nyumba 415 zimebomoka na kusombwa na maji kufuatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha wilayani Uyui mkoani Tabora.
Mkuu wa wilaya hiyo Zuhura Ali amesema hayo wakati akitoa taarifa ya serikali kwenye kikao cha baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya hiyo kilichofanyika Isikizya wilayani humo.
Amesema licha ya kaya hizo kuathirika, jumla ya ekari 225
za mazao mbali mbali zimeaharibiwa vibaya na mvua zinaendelea kunyesha wilayani humo.
Mkuu huyo wa wilaya amesema ekari 342 za tumbaku nazo zimaharibiwa vibaya na mvua hizo.
Amebainisha kuwa mvua hizo pia zimeathiri miundombinu ya barabara au kuyafanya maeneo kutofikika kufuatia barabara kufunikwa na maji.
Kuhusu kaya hizo zilizoathiriwa amesema serikali wilayani
humo imechukua hatua kuhakikisha wakazi wa kaya hizo wanahifadhiwa sehemu zenye
uhakika ili waweze kupata huduma muhimu za kijamii.
Zuhura amesema tayari serikali ngazi ya wilaya imetoa taarifa serikali kuu ili ipatiwe msaada wa dharura kwa ajili ya wahanga hao.
Hata hivyo mkuu huyo wa wilaya amebainisha kuwa ameendelea kutoa elimu kwa wananchi wa wilaya yake kuanza kujenga nyumba imara na wale wengine ambao wamejenga sehemu za mabondeni kuchukua tahadhari ikiwemo kuhama mara moja.
Amesema serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali kwa kufanya ukarabati wa muda maeneo yasiyofikika ili yaweze kupitika kwa kutengeza barabara na madaraja.
Zuhura amesema tayari serikali ngazi ya wilaya imetoa taarifa serikali kuu ili ipatiwe msaada wa dharura kwa ajili ya wahanga hao.
Hata hivyo mkuu huyo wa wilaya amebainisha kuwa ameendelea kutoa elimu kwa wananchi wa wilaya yake kuanza kujenga nyumba imara na wale wengine ambao wamejenga sehemu za mabondeni kuchukua tahadhari ikiwemo kuhama mara moja.
Amesema serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali kwa kufanya ukarabati wa muda maeneo yasiyofikika ili yaweze kupitika kwa kutengeza barabara na madaraja.
No comments:
Post a Comment