Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Tuesday, January 19, 2016

WANAOSHINDWA KULIPIA BILI ZA MAJI WASHITAKIWE KAMA WANAOTAKA KUJINYONGA



 
MKURUGENZI MTENDAJI WA TUWASA MKAMA BWIRE
Na Paul Christian,Tabora

Mamlaka ya maji safi na usafi wa Mazingira Manispaa ya Tabora TUWASA imesema wananchi wanaoshidwa kulipa bili zao za maji kwa wakati na kusababisha kukatiwa huduma wanajikosesha haki ya msingi ya kuishi.

Mkurugenzi mtendaji wa mamlaka hiyo Mkama Bwire amesema baadhi ya wateja wa mamlaka hiyo kutolipia bili zao za  maji kwa wakati walipaswa kushitakiwa kwa kosa la kutaka kujitoa uhai kwa kuwa maji ni uhai.

Mkurugenzi huyo amesema kwa utaratibu wa sasa wateja wa mamlaka hiyo wanaposhindwa kulipia bili zao wanasitishiwa huduma ya maji hali inayopaswa kuangaliwa upya ili iwepo sheria ya kuwashitaki kwa makosa ya kutaka kujitoa uhai kwa kukosa huduma hiyo.

Aidha amewataka wakazi wa Manispaa ya Tabora kuthamini umuhimu wa maji kwa kulipia bili zao, kutunza miundombinu ya maji pamoja na kuhifadhi mazingira.

Awali akizungumza mbele ya madiwani wa halmashauri ya manispaa hiyo mkuu wa wilaya ya Tabora Suleiman Kumchaya amesema wadadisi wa mambo wamebashiri kuwa vita kuu ya tatu ya dunia itasababishwa na uhaba wa maji wakati mahitaji ya binadamu na mifugo yakiongezeka kwa kasi.

No comments: