Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Friday, January 8, 2016

ZAHANATI YA KIJIJI CHA IKOMWA INAKABILIWA NA UPUNGUFU WA DAWA NA VIFAA TIBA



Na Saida Issa, Tabora.

Zahanati ya kijiji cha Ikomwa katika Manispaa ya Tabora inakabiliwa na upungufu mkubwa wa dawa na vifaa tiba hali inayasabisha usumbufu kwa wakazi wanaohudumiwa na zahanati hiyo.

Hayo yamebainishwa na wakazi hao mbele ya diwani wa kata hiyo mheshimiwa Salum Msamazi Lugembe wakati wa ziara ya kutembelea kijiji hicho kwa lengo la kusikiliza kero za wakazi hao.

Hamad Shaban mkazi wa kijiji hicho amesema ukosefu wa vifaa vya kupimia kunawafanya watumishi wa afya kuwapima kwa macho na maelezo ya mgonjwa na kisha kuwapa dawa ya malaria aina ya Mseto hali inayohatarisha afya zao.

Mkazi huyo pia amesema zahanati hiyo inawahudumu wachache wasiokidhi mahitaji ya wagonjwa wanaofika kuhudumiwa.

Mkazi wa Kijiji cha Kapunze katika kata hiyo Amina Juma amebainisha kuwa ukosefu wa barabara ya uhakika inayounganisha kijiji hicho na zahanati kumewasabisha kushindwa kufika kwenye zahanati kufuatia kufunikwa na maji katika kipindi hiki cha mvua zinazoendelea kunyesha.

Amesema hali hiyo inawaathiri sana akinamama wajawazito na watoto wadogo kwa kuwa hawana njia mbadala ya kufikia huduma ya afya na hasa wakati wa dharura.

Akijibu hoja hizo za wananchi diwani wa kata hiyo Salum Msamazi Lugembe amesema kero ya barabara inayounganisha kijiji cha Kapunze na Ikomwa ataifikisha mbele ya kikao cha baraza la madiwani ili itengewe bajeti na kutengenezwa.

Diwani huyo ameanza ziara ya siku mbili ambapo anasikiliza kero za wananchi katika vijiji na  kutembelea taasisi  zilizopo katani humo kabla ya kuanza vikao vya baraza la madiwani wa halmashauri ya manispaa ya Tabora .


No comments: