Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Monday, January 18, 2016

AFISA UPELELEZI WA JESHI LA POLISI SIKONGE AFIKISHWA KIZIMBANI






NA, Thomas Murugwa, Tabora.

Mahakama ya wilaya ya Tabora imemtia hatiani aliyekuwa Afisa upelelezi wa wilaya ya Sikonge Maroba Nyamsongoro na kumtaka ajibu mashitaka mawili ya kuomba na kupokea rushwa yanayomkabili.

Hakimu mkazi mfaidhi wa  mahakama ya wilaya ya Tabora Ngigwana alitoa uamuzi huo Alhamis baada ya kusikiliza maelezo ya ushahidi ya upande wa mashitaka uliokuwa ukiongozwa na wakili Edson Mapalala wa Taasisisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini TAKUKURU.

Ngigwan alisema kuwa upande wa mashitaka umeweza kuthibitisha makosa ya mshitakiwa huyo hivyo anapaswa kutoa utetezi ambao unaweza kumuokoa asipewa adhabu. 

Awali wakili Mapalala aliiambia mahakama hiyo kuwa mshitakiwa alitenda makosa hayo mawili  tarehe 12 Machi,2013 wakati akiwa ni afisa upelelezi wa wilaya ya Sikonge.

Mapalala alisema kuwa siku hiyo mshitakiwa akiwa ni mtumishi wa serikali aliomba Tshs. 2,000,000/= toka kwa Yusuph Hemed ili asimchukulie hatua za kisheria  kwa tuhuma  za kujihusisha na vitendo vya ugaidi.

Katika shitaka la pili ilidaiwa kwa afisa upepelezi huyo wa polisi alipokea kiasi cha Tsh. 700,000/= toka kwa malipo ya awali ili asimchukulie hatua za kisheria.

Mshitakiwa katika kesi hiyo anawakilishwa na  wakili wa kujitegemea Mugaya Mtaki.

No comments: