OPERESHENI ENTEBBE
Paul Christian, Tabora.
Ilikuwa majira ya saa tano usiku wa tarehe 3 Julai 1976 makomandoo
wapatao 100 wa jeshi la Israel (IDF) walivamia uwanja wa Ndege wa kimataifa wa
Entebbe nchini Uganda na kuwakomboa mateka wenye asili ya Israel waliokuwa
wakishikiliwa kwenye moja ya majengo ya uwanja huo.
Uvamizi huo wa jeshi la Israel ulipewa
jina la Operesheni Entebbe au Thunderbolt
au Yonatan “Jonathan” kwa kumbukumbu ya luten Kanali Yonatan
Netanyahu askari pekee wa Isarel aliyeuawa kwenye operation hiyo.
Wiki moja kabla ya operesheni hiyo tarehe 27 Juni, 1976 ndege ya abiria Air
France 139,
aina ya Airbus A300B4-203,
yenye namba za usajili F-BVGG (c/n 019), ilikuwa ikisafiri kutoka Ben Gurion,Israel kuelekea Charles De Gaulle,Ufaransa
kupitia
Ellinikon,Ugiriki
ilitekwa nyara.
Ndege hiyo ilikuwa na abiria 248 na wafanyakazi 12 ilitekwa nyara na
wapiganaji wa kundi la ukombozi wa wapalestina yaani Popular Front
for the Liberation of Palestine – External Operations (PFLP-EO) kwa amri ya
kiongozi wa kundi hilo Wadie Haddad.
Kundi hilo la
PFLP-OE lilijitenga kutoka kundi mama la
Popula Front for the Liberation of Palestine PFLP lililokuwa likiongozwa na
George Habash.
Ndege hiyo ilitekwa
Nyara na wapiganaji hao baada ya kutua kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa Ellinikon jijini
Athens, Ugiriki
ambapo abiria 58 wakiwemo wateka nyara wanne walipanda.
Mara baada ya kuondoka
kwenye uwanja huo wateka nyara hao waliibuka na kuwataka marubani kuiongoza
ndege hiyo kuelekea Benghazi Nchini Libya ambapo ilikaa kwa saa saba kwa ajili
ya kuongeza mafuta.
Ndege hiyo ikiwa Benghazi, watekaji
hao walimwachia huru mateka mmoja mzaliwa wa uingereza mwenye uraia wa Israel
Patricia Martell ambaye alijifanya ameharibu ujauzito wake kwa mshituko.
Hatimaye Ndege
hiyo ya Air France 139 iliondoka Benghazi na kutua kwenye uwanja wa ndege wa kimaitaifa wa
Entebbe nchini Uganda majira ya saa 9 na dakika 15
Alasiri siku ya tarehe 28 Juni, 1976.
Rais wa Uganda Idd
Amin binafsi aliwaunga mkono watekaji hao na kuwakaribisha kwenye ardhi ya
Uganda.Aliwatembelea mara kwa mara na kuwaambia mateka hatua za mazungumzo ili waachiwe
huru.
Mnamo tarehe 28
Juni, 1976 Wateka Nyara hao wanne ambao
wawili wakiwa wapalestina na wengine wawili wakiwa wajerumani wanachama wa
kundi la German Revolutinary Cells, walitoa madai yao kwa serikali ya Israel.
Katika madai
yao watekaji hao walitaka kuachiliwa huru wafungwa 40 wakiwemo wanamgambo wa
kipalestina waliofungwa kwenye magereza ya nchini Israel.
Pili, walitaka
kuachiwa huru kwa wafungwa wengine 13 waliofungwa kwenye magereza ya mataifa
mengine manne.
Tatu,walitaka
kulipwa kiasi cha dola za kimarekani milioni 5 kwa ajili ya kuiachia huru ndege
hiyo ya Air France 139 na kwamba madai hayo yalipaswa kutekelezwa hadi kufikia
tarehe 1 Julai, 1976.
Ndege hiyo
ilipotua kwenye uwanja huo wa Entebbe huku ikilindwa na askari wa jeshi la
Uganda, abiria pamoja na wafanyakazi wote wa ndege hiyo waliamriwa kushuka na
kisha kupelekwa kwenye jengo la zamani lisilotumiwa kwa shughuli za abiria.
Mnamo tarehe 29
Juni, 1976 abiria mateka walitengwa makundi mawili baada ya jeshi la Uganda UDF
kubomoa ukuta uliokuwa ukiwatenganisha chumba cha mapokezi na chumba kingine
katika jengo hilo.
Watekaji
waliwachambua na kuwatenga raia wa Israel wakiwemo raia wa Israel wenye uraia
wa nchi mbili kutoka kwa raia wa nchi nyingine miongoni mwa mateka hao, na raia
hao wa Israel waliamriwa kuingia kwenye chumba kimoja.
Aidha mateka
wasio kuwa raia wa Israel waumini wa madhehebu ya Orthodox wanandoa wanne
kutoka Marekani na Ubelgiji, na Mfaransa mkazi wa Israel waliunganishwa kwenye
kundi lililotengwa la waisrael.
Kwa mujibu wa aliyekuwa
mmoja wa mateka hao watano mfaransa Monique Epstein Khalepski alisema walichukuliwa
na watekaji kwa ajili ya mahojiano kwa kuwahofiwa kuficha utambulisho wa uraia
wao.
Naye Mateka
Mfaransa Michel Cojot-Goldberg alisema watekaji walishindwa kumtambua muisrael
mateka aliyekuwa afisa wa jeshi mwenye uraia wa nchi mbili baada ya kuonesha paspoti
isiyokuwa ya Israel na baadae aliondoka na kundi la pili la mateka walioachiwa huru.
Raia wa
Marekani Janet Almog, Mwanamke Mfaransa Jocelyne Monier ambaye mwenzi wake
alikuwa muisrael, na Jean-Jacques Mimouni mwenye uraia wa nchi za Ufaransa na Israel
ambaye jina lake halikuitwa kwenye orodha ya majina ya abiria, walichagua kwa
hiari zao kujiunga na kundi la mateka wa Israel.
Tarehe 30 Juni,
1976 watekaji waliwaachia huru mateka 48
kutoka kwenye kundi la mateka wasiokuwa raia wa Waisrael ambao wengi wao
walikuwa wazee, wagonjwa, wakinamama na watoto.
Mateka 47 kati
yao walisafirishwa kueleka Paris, Ufaransa, na abiria mmoja Dora Bloch mwenye umri wa miaka 75 alipelekwa hospitali nchini Uganda
kutokana na hali yake ya afya kuwa mbaya.
Tarehe 1 Julai,
1976 ilikuwa siku ya mwisho iliyotolewa na watekaji hao ili madai yao
yatekelezwe, serikali ya Israel ilikubali kufanya mazungumzo kuhusu madai ya
watekaji.
Kutokana hali
hiyo watekaji wakaongeza siku za mazungumzo na kwamba siku ya mwisho ya
utekelezaji wa madai yao ikawa majira ya mchana ya tarehe 4 Julai, 1976.
No comments:
Post a Comment