Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Saturday, January 23, 2016

WAKAZI WA KATA YA NG'WANDE WATUMIA MITUMBWI KUVUKA ENEO LA MTO


Na Ezra Kigata,Ulyankulu.

Wakazi wa vijiji vya kata ya Ng’wande tarafa ya Ulyankulu wilaya ya Kaliua mkoani Tabora wanatumia mitumbwi kuvuka kwenda ng’ambo ya pili kufuata huduma muhimu za kijamii  kufuatia mto Igombe kujaa maji katika kipindi hiki cha mvua.

Wakazi hao wanavushwa kwa mitumbwi kwa gharama ya shilingi 2,000/- kwa mtu mmoja, kuvusha pikipiki wanalipa shilingi 4,000/- hali ambayo inawaathiri kiuchumi.

Simon Michael ni mmoja wa watu wanaofanya kazi ya kuwavusha watu, vyombo vya usafiri na mizigo katika mto huo amesema kazi hiyo inamuingizia kipato kinachomsaidia kukidhi mahitaji ya familia.

Hali hiyo inawaathiri zaidi wanawake, watoto, wagonjwa na wafanyabiashara na wakazi wa kata hiyo wameitaka serikali kuwajengea daraja kwa kuwa kimekuwa kilio chao cha muda mrefu.

No comments: