Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Sunday, January 31, 2016

MALI, GUINEA ZATINGA NUSU FAINALI MICHUANO YA CHAN 2016



 
ALIOU DENG AKISHANGILIA
Na Paul Chriatian.
Timu ya taifa ya Mali imefuzu kucheza nusu fainali ya michuano ya CHAN 2016 kufuatia kupata ushindi wa goli 2 kwa 1 dhidi ya Tunisia katika mechi ya robo fainali iliyochezwa Jumapili.

Alikuwa Mohamed Ali Moncer aliyeipatia Tunisia goli la kuongoza kunako dakika ya 14 ya kipindi cha kwanza baada ya kuunganisha krosi iliyochongwa na Saad Bguir.

Katika kipindi cha pili penati iliyopigwa na Aliou Dieng kufuatia Zied Boughattas kufanyiwa madhambi  ilizaa goli la kusawazisha kwa timu ya Mali.

Kunako dakika ya 80 ya mchezo Diarra akitokea wing ya kushoto aliingia kwenye penati box na kupiga mpira uliompita golikipa wa Tunisia Jerid na kutumbukia nyavuni na kuandika goli la pili kwa Mali.

Hadi mwamuzi wa kati anamaliza pambano hilo Mali waliibuka na magoli 2 kwa 1 dhidi ya Tunisia.

Siku ya Alhamisi Mali itashuka dimbani kuvaana na majirani zao Ivory Coast katika mechi ya nusu fainali.

Fainali itachezwa siku ya Jumapili ijayo.

GUINEA WAKISHANGILIA
Wakati huo huo
timu ya taifa ya Guinea imefanikiwa kucheza nusu fainali ya michuano ya CHAN 2016 baada ya kuwabwaga wapinzani wao Zambia kwenye mechi ya robo fainali iliyochezwa Jumapili kwa jumla ya penati 5 kwa 4.

Mechi hiyo iliyochezwa kwenye uwanja wa Umuganda, Rubavu, timu zote zilimaliza dakika 90 za kawaida bila kufungana na mwamuzi wa kati raia wa Ethiopia Bamlak Tessema aliongeza dakika 30 ambapo zilimaliza bila kufungana kwa mara nyingine.

Mikwaju ya penati iliamuliwa  ili apatikane mshindi, Guinea walifunga penati zao kupitia kwa Ibrahima Bangoura, Mohamed Thiam, Issiaga Kamara, Ibrahima Soumah na goalkeeper Abdol Azizi Keita ambapo Douda Kamara na Ibrahim Sankhin walipoteza penati zao.

Kwa upande wa Zambia, Buchizya Mfuma, Spencer Sautu,Cleotus Chama na Adrian Chama waliwafanyikiwa kukwamisha nyavuni penati zao, huku Christopther Katongo, Stephene Kabamba na Daut Musekwa wakikosa penati zao.

Kwa ushindi huo Guinea itakutana na Congo DR katika mechi ya nusu fainali itakayochezwa siku ya Alhamisi wiki hii.

No comments: