Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Tuesday, January 19, 2016

ASKARI POLISI WILAYANI KALIUA WAACHE KUVUJISHA TAARIFA ZA SIRI


IGP ERNEST MANGU

Na Paul Christian,Kaliua

Askari polisi wa wilaya ya Kaliua mkoani Tabora wameaswa kuacha tabia ya kuvujisha taarifa za siri kuhusu wahalifu wanazopewa na raia wema ili kukabiliana na matukio ya uhalifu wilayani humo.

Rai hiyo imetolewa hivi karibuni na mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kaliua Haruna Kasele alipokuwa akizungumza na askari polisi wa tarafa ya Ulyankulu wilayani humo.

Amesema baadhi ya askari hao wamekuwa na tabia ya kuvujisha kwa watuhumiwa taarifa za siri wanazopewa na wananchi jambo ambalo limehatarisha maisha na mali za raia hao kwa kulipiziwa visasi.

Kasele amesema vitendo hivyo ambavyo ni kinyume na maadili ya jeshi la polisi vimekuwa vikiwasaidi wahalifu kuharibu au kuficha ushahidi  na hivyo raia wema kuonekana waongo.

Mwenyekiti huyo wa halmashauri amesisitiza kuwa endapo askari polisi wilayani humo watafanya kazi kwa misingi ya maadili wananchi wako tayari kutoa ushirikiano wa kuwafichua wahalifu.

No comments: