Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Sunday, January 3, 2016

WATU WAWILI WAENDA JELA MIAKA 60 WILAYANI URAMBO



Na Lucas Raphael,Urambo

Watu wawili kati ya sita wamehukumiwa kifungo cha jumla ya miaka 60 jela baada ya kupatikana na hatia ya unyang’anyi wa kutumia  silaha aina ya bastola na kupora kiasi cha shilingi 380,000/=.

Akitoa hukumu hiyo hakimu mkazi wa mahakama  wilaya ya Urambo mkoani Tabora Baptista Kashusha alisema anatoa adhabu hiyo ili iwe fundisho kwa watu wengine wenye nia ya kutenda makosa kama hiyo.

Alisema kwamba kutoakana na kukidhiri kwa vitendo vya uhalifu katika maeneo ya mijini na vijijini adhabu kali ndio fundisho pekee kwa watu wa aina hiyo.

Waliopatikana na hati hiyo ya unyang’anyi wa kutumia silaha aina ya bastola na marungu na kufanyikiwa kupora kiasi hicho cha fedha ni Mageta Jumanne (23) na Mhoja Mabula (27) wote ni wakazi wa Igagala wilaya ya Kaliua.

Hata hivyo mahakama hiyo iliwaachia huru watuhumiwa wanne kwa kukosa ushahidi wa kutosha kuweza kuwatia hatiani ambao ni Amos Mabiika(20) ,Rashid Emanuel (25), Kadoke Msengele(24) Peter Cherehani(38) .

Kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo mwendesha mashitaka wa jeshi la polisi mkaguzi msaidizi Felbet Pima aliomba mahakama hiyo kutoa adhabu kali kwa washitakiwa hao iliwe iwe fundisho kwa watu wengine.

Awali mwendesha mashitaka huyo aliiambia mahakama hiyo kuwa mnamo tarehe 20 Januari 2015 majira ya saa 7 usiku katika  kijiji cha Mtakuja wilaya ya kaliua mkoa wa tabora washitakiwa kwa pamoja kabla na baada ya kupora waliitishia kwa bastola na marungu na kufanikiwa kupora kiasi cha shilingi 380,000/kutoka kwa Regina John.


No comments: