Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Tuesday, January 12, 2016

JESHI LA POLISI MKOANI TABORA LIMEWATAKA MADEREVA KUEPUKA MAKOSA YA KIBINADAMU

EDGAR NA DENNIS (ALIYEVAA HEADPHONE) WATANGAZAJI WA MEZA HURU VOT FM STEREO


RTO MICHAEL DELELI


Na Paul Christian, Tabora.

Jeshi la polisi mkoani Tabora limemewataka madereva wa vyombo vya moto kuepuka kufanya makosa ya kibinadamu ili kuepusha ajali barabarani.

Mkuu wa kitengo cha usalama barabarani  mkoa wa Tabora (RTO), SP Michael Deleli ameyasema hayo leo asubuhi alipokuwa akihojiwa kwenye kipindi cha Meza Huru kinachorushwa na VOT FM STEREO.

Amesema madereva wote wanapaswa kuepuka vitendo vya kunywa pombe kulewa na kuendesha vyombo vya moto,kutokuwa na mafunzo ya udereva,  kuongea kwa simu wakati wanaendesha, kuendesha magari mabovu, kutoheshimu alama za barabarani, kutoheshimu sheria za usalama barabarani pamoja na matumizi sahihi ya taa za vyombo hivyo.

Deleli amebainisha kuwa makosa ya kibinadamu yanayofanywa na madereva wanapokuwa wanaendesha vyombo vya moto yamechangia kutokea kwa ajali ambazo zimesababisha vifo na majeruhi wengi.

Mkuu huyo wa kitengo cha usalama barabarani mkoa wa Tabora amesema katika kukabiliana na hali hiyo mwaka 2015 zaidi ya madereva 900 walipatiwa mafunzo ya udereva kwa kushirikiana na vyuo vya mafunzo ya udereva pamoja na mamlaka ya udhibiti wa usafiri wa nchi kavu na majini SUMATRA.

Aidha amewaonya wamiliki wa magari yanayotoa huduma za usafirishaji mkoani Tabora kuacha tabia ya kubadili muundo wa viti vya magari yao kwa lengo la kubeba abiria wengi pamoja na mizigo.

Deleli amebainisha hatua hiyo ya wamiliki wa magari hayo ni uvunjaji wa sheria za nchi na kwamba hatua za kisheria zitachukuliwa kwa wale watakaobainika.

No comments: