Na Paul Christian, Tabora.
Jumapili
ya tarehe 17 mwezi huu ilikuwa siku ya
kumbukumbu miaka 55 ya kifo cha waziri mkuu wa kwanza wa Jamhuri ya Kidemokrasi
ya Congo Patrice Lumumba.
Patrice
Lumumba alizaliwa Julai 2, 1925 Katakokombe na kuuawa kikatili na kwa maumivu
makali Elisabethville kwa sasa (Lubumbashi) tarehe 17 January,1961 akiwa na
umri wa miaka 35 tu.
Kiongozi
huyo wa kwanza wa taifa hilo aliongoza chama cha Congolese National Movement
MNC.
Kifo
chake kiliratibiwa na kutekelezwa na wakoloni wa taifa hilo Ubelgiji
wakishirikiana na Marekani kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kujihusisha
moja kwa moja na suala la kuomba msaada kutoka Urusi.
Patrice
Lumumba na chama chake kilishinda uchaguzi uliofanyika kuanzia tarehe 11 hadi 25 Mei 1960 na hivyo
Congo DRC kupata uhuru wake tarehe 30 Juni, 1960.
Kiongozi
huyo atakumbukwa kwa msimamo wake, kutokuwa na woga, kupinga ubeberu na kuwa na
wazo la kuiona Afrika huru na siku moja kuwa Taifa moja “The State of Africa”.
No comments:
Post a Comment