Na Paul Christian,
Tabora.
Dokta
Deus Kitapondya wa EFATHA Dispensary mjini Tabora amesema ugongwa wa U.T.I ni
ugonjwa unaoathiri njia ya mkojo na zaidi huwashambulia wanawake kutokana na
sababu za kimaumbile.
Amesema
U.T.I ni kifupi cha Urinary Track Infection
ni ugonjwa ambao unawaathiri pia watoto wadogo.
Amesema ugonjwa huo uathiri mfumo wa
mkojo ikiwa ni pamoja na mirija ya mkojo kutoka kwenye figo (ureter), kibofu
cha mkojo na mrija kwa kupitisha mkojo kutoka kwenye kibofu na kisha kutoka nje ya mwili (urethra).
Dokta Kitapondya amebainisha kuwa
ugonjwa huo pia unaweza kuathiri figo kama hakudhibitiwa mapema.
Amesema ugonjwa huo husababishwa na
bakteria anayeitwa Escherichia coli (E. coli) ambao kwa sehemu kubwa makazi yao
ya kawaida ni kwenye utumbo mpana,
na hivyo huwa wanapatikana pia kwenye haja kubwa.
Aidha amesema bakteria hao wa
Escherichia coli hawasababishi peke yao U.T.I bali huambatana na wengine waitwao
staphylococcus, saprophyti cus, pseudom onas, enterobacter na kadhalika.
Dokta Kitapondya
ameeleza kuwa U.T.I inaambukizwa kwa kutumia vyoo vichafu kwa kuwa ndani ya vyoo
kunabakteria wengi,kutumia maji machafu wakati wa kujisafisha au kuoga, unywaji
wa vinywaji vyenye sukari kwa muda mrefu pamoja na kutokunywa maji ya kutosha.
Amezitaja sababu nyingine kuwa ni
upungufu wa homoni ya wanawake iitwayo Oestrogen husababisha bakteria
wanaosababisha maambukizi katika njia ya mkojo kuzaliana kirahisi.
Mtaalam huyo wa afya ametaja kufanya
ngono na mtu mwenye bacteria wa U.T.I unaweza kuambukizwa.
Dokta Kitapondya amezitaja baadhi ya dalili
za mtu aliyeambukizwa U.T.I kuwa ni maumivu wakati wa kukojoa, mkojo kuwa
na rangi ya njano kupindukia na kuwa na harufu kali ijapokuwa siyo kila mwenye
dalili hizo ana maambukizi katika njia ya mkojo.
Dalili nyingine za U.T.I ni kutokwa na usaha wakati wa kukojoa, kabla au
baada ya kukojoa ukiambatana na maumivu na kuhisi moto wakati mkojo ukitoka.
Amesema baadhi ya watu wenye U.T.I hupata
vichomi katika njia ya mkojo, kuhisi kuwashwa sehemu za siri, kuumwa kiuno au
tumbo na kadhalika.
Dokta Kitapondya ameeleza mgonjwa wa
U.T.I anaweza pia kukumbwa na homa kali ya mara kwa mara,mwili kuwa mchovu na kwa
watoto hupoteza hamu ya kula na mwili huonesha kuchoka.
Amesema wagonjwa wengine hupata maumivu kwenye kibofu cha mkojo ambapo husikia maumivu ya chini ya tumbo usawa wa kitovu yasiyoisha.
Hata hivyo amesema U.T.I hutibika kwa dawa mbalimbali za kisasa baada
ya kufanyiwa vipimo na kuthibitika kuwa mgonjwa ana maambukizi hayo.
Dokta Kitapondya amesisitiza kuzingatia
usafi kwa kujisafisha kwa kutumia maji yaliyosalama, kufanya ngono salama na
kuwaona wataalam wa afya mara unapohisi maambukizi kwenye mfumo wa mkojo.
No comments:
Post a Comment