Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Saturday, January 23, 2016

WATAMBUE WABUNGE WA TABORA NA KAMATI WALIZOPANGIWA NA SPIKA



 
SPIKA WA BUNGE JOB NDUGAI
Na Paul Christian, Tabora

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Job Ndugai ametangaza majina ya wabunge katika kamati  za  kudumu za Bunge la 11 kwa lengo la kutekeleza vyema madaraka yake.

Kwa upande wa wabunge wa mkoa wa Tabora, mbunge wa jimbo la Nzega mjini Mhe. Hussein Mohamed Bashe na mbunge wa jimbo la Urambo Mashariki Mh. Margaret Simwanza Sitta wamepangwa kuwa wajumbe wa kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii.

Mbunge wa Jimbo la Tabora mjini Mhe. Emmanuel Adamson Mwakasaka ni mjumbe wa kamati ya katiba na sheria na mbunge wa viti maalum mkoa wa Tabora Mhe. Munde Abdallah Tambwe amekuwa mjumbe wa kamati ya Hesabu za Serikali (PAC).

Mbunge wa Jimbo la Sikonge Mhe. Joseph George Kakunda pamoja na mbunge wa jimbo la Bukene Mhe. Selemani Jumanne Zeddy wameteuliwa kuwa wajumbe wa kamati ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma ambapo mbunge wa jimbo la Igalula Mhe. Mussa Rashid Ntimizi amepangiwa kamati ya Miundombinu.

Wengine ni mbunge wa jimbo  la Ulyankulu John Peter Kadutu ameteuliwa kuwa mjumbe wa kamati ya Masuala ya UKIMWI na mbunge wa jimbo la Manonga Mhe. Seif Khamis Said Gulamali amepangiwa kuwa mjumbe wa kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC).

Mbunge wa Jimbo la Tabora Kaskazini Mhe. Almas Athuman Maige ameteuliwa kuwa mjumbe wa kamati ya Sheria Ndogo ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ambapo Mbunge wa jimbo la Igunga  Mhe. Dkt Dalali Peter Kafumu amekuwa mjumbe wa kamati ya Viwanda, Biashara na Mazingira.

Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Tabora Mwanne Ismail Mchemba amepangiwa kamati ya Utawala na Serikali za Mitaa na mbunge wa jimbo la Kaliua Mhe. Magdalena Hamis Sakaya amekuwa mjumbe wa kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya Kanuni  za Bunge.



No comments: