Na Deogratius Yagomba, Tabora.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya maarufu kama “bongo
fleva” Baraka da Prince amesema anaamini ataendelea kuzikonga nyoyo za
mashabiki wa muziki huo kwa mwaka 2016.
Kauli hiyo ya kujiamini ameitoa Jumamosi wakati akifanya mahojiano ya moja kwa moja kwa
njia ya simu katika kipindi cha Weekend Blast kinachorushwa na VOT FM STEREO
kuanzia majira ya saa 4:15 hadi saa 7:00 usiku kila Jumamosi.
Msanii huyo anayetamba na vibao mbalimbali amesema
katika kukoleza ladha ya muziki wake ameamua kutengeneza video mpya na
mtayarishaji kutoka nchini Kenya Kelvin Bosco na ameiachia terehe 16 mwezi huu.
Baraka da Prince ametamba na vibao mbalimbali
ikiwemo Jichunge, So fine,Siachani nawe na Nivumilie ambacho amemshirikisha
msanii wa kike Ruby.
Weekend Blast ya VOT FM STEREO inamtakia kila la
heri msanii huyo katika kufikia kilele cha mafanikio.
No comments:
Post a Comment