Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Saturday, January 2, 2016

CHAMA CHA WANANCHI CUF: MAGUFULI ANATEKELEZA SERA ZA UKAWA


Rais wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli

 Na Hastin Liumba,Kaliua

CHAMA cha wananchi (CUF) wilaya ya Kaliua mkoani Tabora kimempongeza Rais John Magufuli kwa  kutekeleza sera za upinzani.

Mwenyekiti wa CUF wilaya ya Kaliua Lubaga Katwiga alisema hayo wakati akiongea na waandishi wa habari wilayani humo.

Katwiga alisema hatua anazochukua Rais Magufuli kwa sasa zilikuwa ni sehemu ya sera na ilani ya vyama vilivyokuwa vinaunda umoja wa katiba ya wananchi UKAWA.

 Alisema endapo UKAWA ungeshinda uchaguzi wa Oktoba 25,2015 hayo anayoyafanya Magufuli yangetekelezwa na wao ikiwa ni sehemu ya kushughulikia kero za wananchi.

Aidha mwenyekiti huyo alichukua nafasi hiyo kuwapongeza wananchi wa jimbo la Kaliua kwa kumchagua mbunge toka chama cha wananchi CUF Magdalena Sakaya.

Katwiga alisema mbunge huyo ni chaguo sahihi kwa wanakaliua kwani ni mtu makini na mfuatiliaji wa kero za wananchi na kuzipatia ufumbuzi.

Mwenyekiti huyo wa CUF alisisitiza kuwa wananchi wa jimbo hilo watarajie mabadiliko ya kiuchumi, kisiasa na kijamii chini ya uongozi wa mbunge huyo na kwamba hawatajuta kumchagua.





No comments: