![]() |
Rais wa awamu ya tatu Benjamin William Mkapa |
Na Paul Christian, Tabora.
Waandishi
wa habari mkoani Tabora wameaswa kuongeza maarifa na ufahamu kwa kusoma vitabu
na machapisho mbalimbali ili kuongeza tija katika kazi zao za kuhabarisha,
kujulisha na kuburudisha.
Mkuu
wa wilaya ya Tabora Suleiman Kumchaya amesema hayo alipokua akizungumza na
waandishi wa habari ofisini kwake katika kuutathimini mwaka 2016 na tasnia
hiyo.
Amesema,
“Kusoma sana kunaongeza uwezo wa kufahamu na kuchambua mambo mbalimbali kwa
kina, hali hii itawafanya waandishi wa habari kutekeleza majukumu yao kwa
ufanisi zaidi kuliko ilivyosasa.”
Mkuu
huyo wa wilaya amehimiza waandishi hao kutopuuza suala la kusoma kwa kuwa mwaka
2016 utakuwa wa mabadiliko katika Nyanja za kiuchumi,kisiasa,kijamii na
kiutamaduni na kwamba uchambuzi yakinifu wa waandishi hao utasaidia kuharakisha
mabadiliko hayo.
Kumchaya
amewataka waandishi hao kuiga mfano wa Rais wa awamu ya tatu Benjamin William
Mkapa ambaye muda wake mwingi anautumia kusoma vitabu na machapisho mbalimbali hata
wakati akiwa Rais wa nchi.
“Mzee
Mkapa akiwa kiongozi wa nchi hakupenda vitu vya anasa hata anapokuwa nje ya
nchi muda mwingi aliutumia kusoma vitabu.” amesema mkuu huyo wa wilaya.
Kumchaya
ambaye aliwahi kuwa msaidizi wa Rais huyo wa awamu ya tatu amesema, “ukitaka
kuelewana na mzee Mkapa mwambie nimeona kitabu kizuri mahali fulani na sio
viatu vizuri au vitu vya anasa.”
Suleiman
Kumchaya amewahi kufanyakazi kwenye shirika la utangazaji Tanzania TBC zamani likijulikana
kama Radio Tanzania na idhaa zake mbalimbali.
Rais
wa awamu ya tatu Benjamin Mkapa ni mwandishi wa habari na amewahi kuwa
mwandishi wa Rais wa awamu ya kwanza Mwl. Julius Kambarage Nyerere.
No comments:
Post a Comment