Na Ramadhan Faraji, Tabora.
Ligi daraja la kwanza
imeendelea kushika kasi Jumapili kufuatia timu ya Polisi Tabora
kuikaribisha timu ya Geita Gold Mine kwenye uwanja wa Ally Hassan Mwinyi mjini
Tabora.
Mechi hiyo iliyokuwa na
ushindani mkubwa iliwasisimua mashabiki wa Polisi Tabora ambao walikuwa na
shahuku ya kuiona timu yao ya nyumbani ikifanikiwa kuondoka na pointi 3 muhimu
na kujiweka kwenye nafasi nzuri ya kupanda ligi kuu ya Tanzania Bara.
Iliwachukua dakika 81
Polisi Tabora kupitia kwa mchezaji wao Ked Mohamed kuwanyanyua mashabiki wao
baada ya kupachika bao la kwanza na la ushindi.
Kwa ushindi huo
Polisi Tabora imefikisha pointi 24 sawa na wapinzani wao Geita Gold Mine ambao
wanaongoza ligi hiyo wakiwa na pointi 24 na wakiwa na tofauti ya goli moja.
Polisi Tabora ambayo
inanyemelea nafasi ya kucheza ligi kuu Tanzania Bara pamoja na wapinzani wao
Geita Gold Mine wamebakiza mechi mbili kila timu ili kukamilisha mzunguko wa pili wa
ligi daraja la kwanza ambao utaamua timu ipi ipande daraja.
Mwishoni mwa wiki
hii Polisi Tabora watawafuata maafande JKT Kanembwa huko Kigoma wakati Geita Gold Mine watawafuata
maafande wa JKT Oljoro mjini Arusha.
Tabora Watch
inawatakia kila la heri Polisi Tabora kwenye mbio hizo za kupanda daraja.
Wakati huo
huo
siku ya Jumamosi Rhino Rangers ya Tabora ikiwa kwenye uwanja wa ugenini mjini Musoma
ilipoteza mechi yake mbele ya maafande wa Polisi Mara baada ya kukubali kichapo
cha bao1 kwa 0 ikiwa ni mwendelezo wa ligi daraja la Kwanza.
No comments:
Post a Comment