![]() |
SHAMBA LA TUMBAKU |
Na Paul Christian, Nkinga.
Chama
Kikuu cha Ushirika wa Wakulima wa Tumbaku kanda ya Magharibi WETCU Ltd
kimeazimia kupigania kushuka kwa bei ya mbolea na kuongezeka kwa bei ya Tumbaku
ili mkulima anufaike na zao hilo.
Azma
hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Chama hicho Mkandala Gabrie Mkandala alipofanya
mahojiano maalumu na VOT FM STEREO akiwa kwenye hospitali ya rufaa Nkinga
wilaya ya Igunga mkoani Tabora.
Amesema
lengo la Chama hicho kwa sasa nikuhakikisha mkulima wa zao hilo anapata unafuu
wa bei ya mbolea ili aweze kulima kilimo chenye tija kwa kuwa hilo
linawezekana.
Mkandala
amebainisha kuwa azma ya WETCU Ltd kwa sasa ni kupigania bei ya Tumbaku ipande
kutoka hapa ilipo sasa hali itakayomfanya mkulima kuona mapato yanaendana na
uwekezaji wa nguvu, akili, muda na fedha katika kilimo cha Tumbaku.
Aidha
mwenyekiti huyo amesema kwa mwaka huu WETCU Ltd imejipanga kumfanya mkulima wa
zao hilo kuendana na kalenda ya zao kwa kuanza masoko mapema ili yakamilike
kati ya mwezi wa sita na wa saba.
Mkandala
amesema masoko yakikamilika mapema wataweza kujua idadi na mahitaji ya Vyama
vya Msingi vya Ushirika hatua itakayosaidia kuvipelekea mbolea mapema kati ya
mwezi wa Nane au wa Tisa.
Amesisitiza
kuwa WETCU Ltd imejipanga kuondoa kero ya ucheleweshaji wa pembejeo kwa
wakulima wa zao hilo jambo linalowaumiza sana.
Mwenyekiti
huyo wa WETCU Ltd amebainisha kuwa tayari kiwanja kilichotengwa kwa ajili ya
ujenzi wa kiwanda cha Tumbaku wilayani Urambo kimepitishwa na wizara husika na
hivyo kuwafanya waanze mchakato wa ujenzi.
Ametaja
baadhi ya mikakati ya uwekezaji inayotarajiwa kuanza utekelezaji wake mwaka huu
kuwa ni pamoja na ujenzi wa jengo la ghorofa WETCU Plaza ambalo litakuza mapato
ya chama hicho.
No comments:
Post a Comment