Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Sunday, January 10, 2016

KITUO CHA AFYA ULYANKULU CHAONGOZA KWA NIDHAMU NA USAFI WILAYANI KALIUA



Wakazi wa Tarafa ya Ulyankulu wakiwa kwenye kituo cha afya Ulyankulu

Na Paul Christian, Ulyankulu.

Kituo cha afya cha Ulyankulu kimeelezwa kuwa cha mfano wilayani Kaliua kwa kutolalamikiwa na wananchi kuhusu huduma zake.

Kauli hiyo ilitolewa na mbunge wa jimbo jipya la Ulyankulu wilayani humo John Peter Kadutu akiungwa mkono na mwenyekiti wa kamati ya elimu, afya na maji ya halmashauri ya wilaya ya Kaliua ambaye pia ni diwani wa kata ya Uyowa katika tarafa ya Ulyankulu Alphonce Msanzya.

Mbunge huyo amesema hajawahi kupokea malalamiko juu ya huduma zinazotolewa katika kituo hicho cha afya licha ya kukabiliwa na changamoto mbalimbali.

“Tangu nikiwa diwani wa kata ya Ichemba na baadaye mwenyekiti wa kwanza wa halmashauri ya wilaya ya Kaliua, sijawahi kupokea malalamiko ya aina yoyote kutoka kwa wananchi kuhusu huduma zenu.” Amesema kiongozi huyo.

Kadutu amebainisha kuwa  zahanati iliyoko katika kijiji anachoishi cha Ichemba imekuwa ikilalamikiwa kwa huduma zake tofauti kabisa na kituo hicho cha afya ambacho kinahudumia watu wengi.

Aidha ameupongeza uongozi wa kituo hicho cha afya kwa kuzingatia usafi kwa kuyafanya mazingira kuwa nadhifu wakati wote bila kujali wakati wa ujio wa wageni.
Kaimu Mganga Mfawidhi Lazaro Jeremia (aliyeinua mikono) akifafanua Jambo
Kaimu mganga mfawidhi wa kituo hicho cha afya Lazaro Jeremia amesema kituo hicho kinakabiliwa na changamoto kadhaa ikiwemo ukosefu wa maji ya uhakika,umeme,upungufu wa dawa, vifaa tiba, watumishi,kutokuwa na huduma ya kuongeza damu,ubovu wa barabara inayoelekea katika kituo hicho pamoja na stahili za watumishi.



No comments: