Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Sunday, January 17, 2016

MUSA NTIMIZI:AKABIDHI ZAWADI KWA WASHINDI WA LIGI DARAJA LA NNE WILAYA YA UYUI



 
MBUNGE WA IGALULA MUSA NTIMIZI AKIWAPA MKONO WACHEZAJI WA TIMU YA WEMBE FC
Na Paul Christian, Kigwa.

Timu za soka za wilaya ya Uyui mkoani Tabora zilizofuzu kushiriki ligi daraja la tatu ngazi ya mkoa zimetakiwa kujianda kwa mazoezi, kisaikolojia,kuzielewa na kuzitafsiri sheria za mchezo huo ili kuondoa malalamiko yasiyo na msingi.

Agizo hilo limetolewa na Mbunge wa jimbo la Igalula ambaye pia ni mwenyekiti wa chama cha soka wilaya ya Uyui  Musa Ntimizi wakati akikabidhi zawadi kwa washindi wa ligi daraja la nne wilayani humo iliyomalizika mwishoni mwa wiki  ambapo Kigwa FC waliibuka washindi.

Mbunge huyo amesema timu hizo zikijiandaa vyema zitaenda kushindana na sio kushiriki katika ligi daraja la tatu kwa kuwa wanakwenda kukutana na waamuzi wenye uzoefu na waliobobea kwenye mchezo huo.

Katika hafla hiyo fupi Musa Ntimizi alitoa zawadi ya shilingi 250,000/- na Kombe kwa timu ya Kigwa FC ambayo iliibuka kinara wa ligi daraja la nne wilayani humo baada ya kuichapa pasipo huruma timu ya Wembe FC ya kata ya Usagari kwa jumla ya mabao 6 kwa 2 kwenye mechi ya fainali.

Hata hivyo waswahili walisema mgaa gaa na upya hali wali mkavu Wembe FC ilizawadiwa shilingi 150,000/- kwa kushika nafasi ya pili huku Manchester United ya Igalula ikiambulia shilingi 100,000/- kwa kuwa washindi watatu.

Aidha Musa Ntimizi ametoa zawadi ya mipira yenye kiwango na ubora unakubaliwa na shirikisho la soka Duniani FIFA kwa timu zote zilizofuzu kushiriki ligi daraja la tatu pamoja na kuahidi kuzilipia ada ya ushiriki wa ligi hiyo.

Mbogo Zyagi mchezaji wa nafasi ya ushambuliaji wa timu ya Kigwa FC aliibuka mfungaji bora kwa kuzifumania nyavu mara 11 alipokutana na timu pinzani tangu kuanza kwa ligi hiyo Januari 6 mwaka huu na alizawadiwa shilingi 50,000/- taslimu.

Awali hafla hiyo ya kutoa zawadi ilitanguliwa na mechi ya fainali iliyozikutanisha Kigwa FC na Wembe FC ya kata ya Usagari jimbo la Tabora Kaskazini ambapo Wembe ulikosa makali na kukubali kichapo cha mabao 6 kwa 2 kutoka kwa Kigwa FC.

Magoli ya Kigwa FC yalipachikwa nyavuni na Mbogo zyagi magoli 3, Hassan Juma goli 1, Devid Eliasi goli 1 na Ali Kassimu goli 1 na yale ya upande wa Wembe FC yalifungwa na Seleman Salum na Hamis Maige.

Ligi hiyo ya daraja la nne imegharimu kiasi cha shilingi milioni 6 zilizotolewa na Mbunge wa Igalula Musa Ntimizi ambazo ziligharamia ada za timu zote 13 zilizoshiriki, gharama za usafiri, gharama za waamuzi kutoka Tabora manispaa, gharama za mipira, kombe , gharama za maofisa wasimamizi wa ligi hiyo na nyingine.

Wilaya ya Uyui itawakirishwa na jumla ya timu 5 katika ligi daraja la tatu ngazi ya mkoa ambapo Kigwa FC,Wembe FC na Manchester United ya Igalula zinaungana na timu nyingine mbili ambazo ziko katika ngazi hiyo ya daraja la tatu.

No comments: