Na Paul Christian, Kaliua.
Wakazi wa kitongoji cha Uswahilini kijiji cha
Ibambo kata ya Mwongozo wilayani Kaliua wamekumbwa
na mafuriko kufuatia mvua kubwa iliyonyesha katika maeneo hayo na kuharibu vitu
mbalimba ikiwemo nyumba, chakula na mazao kwenye mashamba.
Akizungumza na VOT FM STEREO kwa njia ya simu mwenyekiti
wa kijiji cha Ibambo Ngomba R. Ngomba
amesema mafuriko hayo yamezikumba nyumba 30 na kumi kati ya hizo zimeharibiwa
vibaya.
Amesema nyumba hizo 10 zilizoharibika zilikuwa
zikikaliwa na watu 90 ambao kwa sasa wamehifadhi na majirani.
Ngomba amebainisha kuwa mafuriko hayo yameharibu
chakula kilichokuwa kimehifadhiwa katika nyumba hizo hali inayosabisha familia
hizo kuhitaji msaada wa dharura wa chakula na mahitaji mengine ya kibinadamu.
Mwenyekiti huyo ameeleza kuwa mafuriko hayo
yameharibu mimea mashambani ikiwemo mpunga ekari 60, mahindi ekari 30,viazi
vitamu ekari 15, karanga ekari 22, tumbaku ekari 3, mihogo ekari 1, alizeti
ekari 1 na kunde ekari 5.
Ameyataja madhara mengine yaliyojitokeza ni uharibifu wa chakula kilichokuwa kimehifadhiwa kwenye kaya zilikumbwa na mafuriko kuwa ni magunia 24 ya mpunga, mahindi magunia 30, viazi vitamu vilivyokaushwa (matobolwa) magunia 20,karanga magunia 13, magunia matano ya maharage, kilo 400 za mchele na magunia matatu ya kunde.
Ameyataja madhara mengine yaliyojitokeza ni uharibifu wa chakula kilichokuwa kimehifadhiwa kwenye kaya zilikumbwa na mafuriko kuwa ni magunia 24 ya mpunga, mahindi magunia 30, viazi vitamu vilivyokaushwa (matobolwa) magunia 20,karanga magunia 13, magunia matano ya maharage, kilo 400 za mchele na magunia matatu ya kunde.
Ngomba ameyataja madhara mengine yaliyosababishwa
na mafuriko hayo ni vifo vya ng’ombe wawili na mbuzi watatu.
Mwenyekiti huyo wa kijiji cha Ibambo amesema tathimini ya uharibifu wa mazao na chakula imejumuisha kaya na maeneo yote yaliyoathiriwa na mafuriko katika kitongoji cha Uswahilini.
Mwenyekiti huyo wa kijiji cha Ibambo amesema tathimini ya uharibifu wa mazao na chakula imejumuisha kaya na maeneo yote yaliyoathiriwa na mafuriko katika kitongoji cha Uswahilini.
Mwenyekiti huyo ametoa wito kwa kamati ya maafa
ngazi ya wilaya ya Kaliua kuwapelekea msaada wa chakula na mahitaji mengine ya
ziada wakazi hao walioathirika na mafuriko.
Wakati huo huo mto Wala umefurika maji katika eneo la Kasisi kata ya Pangale wilaya ya Sikonge mkoani Tabora na kusababisha eneo la daraja katika eneo hilo kuharibika na kusababisha magari ya abiria na mizigo yanayotumia barabara ya Tabora-Sikonge kukwama katika eneo hilo.
Wakati huo huo mto Wala umefurika maji katika eneo la Kasisi kata ya Pangale wilaya ya Sikonge mkoani Tabora na kusababisha eneo la daraja katika eneo hilo kuharibika na kusababisha magari ya abiria na mizigo yanayotumia barabara ya Tabora-Sikonge kukwama katika eneo hilo.
No comments:
Post a Comment