Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Friday, January 15, 2016

MKANDALA AFANYIWA UPASUAJI MGUU WAKE WA KUSHOTO



KATIBU WA SIASA,ITIKADI NA UENEZI WA CCM WILAYA YA UYUI SAID SADALA KATALA AKIMJULIA HALI MWENYEKITI WA WETCU Ltd MKANDALA GABRIEL MKANDALA AMBAYE AMELAZWA HOSPITALI YA RUFAA NKINGA WILAYA YA IGUNGA MKOA WA TABORA BAADA YA KUPATA AJALI YA GARI JANUARI 6 2016

Na Paul Christan, Tabora.

Mwenyekiti wa Chama Kikuu Cha Ushirika wa Wakulima wa Tumbaku Kanda ya Magharibi WETCU Ltd Mkandala Gabriel Mkandala amefanyiwa upasuaji wa mguu wake wa kushoto kufuatia ajali aliyoipata Januari 6 mwaka huu.

Akizungumza na VOT FM STEREO akiwa kitandani alipolazwa kwenye hospitali ya rufaa ya Nkinga wilayani Igunga mkoani Tabora mwenyekiti huyo amesema upasuaji huo umefanyika Alhamisi wiki hii kuanzia majira ya saa saba mchana hadi saa mbili usiku.

Mkandala amebainisha kuwa upasuaji huo umefanyika baada ya mguu huo wa kushoto kuvunjika katika tukio hilo la ajali ambapo gari yake iliyokuwa ikitokea Usoke wilayani Urambo kuelekea Tabora mjini kuligonga trekta ambalo halikuwa na taa wala kiakisi mwanga katika maeneo ya Tumbi barabara kuu ya Tabora- Urambo.

Aidha mwenyekiti huyo amesema katika ajali hiyo pia alivunjika mkono wake wa kushoto mara mbili ambao nao utafanyiwa upasuaji siku chache zijazo baada ya kupona majeraha yaliyotokana na kuchomwa na vyuma pamoja na vioo.

Amesema, “tukiwa tumelikaribia trekta lile ghafla nikaijiwa na fikra kuwa tunakwenda kuligonga nikamwambia dereva tunagonga, lakini katika dakika hiyo hiyo nikasikia kishindo kikubwa.”amesema Mkandala.

Mwenyekiti huyo wa WETCU Ltd amebainisha kuwa wakati ajali inatokea alikuwa na akili zake timamu licha ya kuwa alibanwa kiasi cha kuhitaji msaada wa kutolewa aliweza kupiga simu kwa mkuu wa mkoa Ludovick Mwananzila na familia yake kuwajulisha tukio hilo.

“Jambo la kushangaza dakika chache baada ya ajali kutokea walifika majirani zangu wawili ambao ninaishi nao nyumbani Usoke hali iliyonipa matumaini ya kuwa salama zaidi japo nilikuwa bado nimenasa kwenye gari.”ameeleza Mkandala.

Amesema, “kama binadamu ninapaswa kumshukuru mungu kwa kila jambo hata kwa hili namshukuru mungu.”

Mwenyekiti huyo amewashukuru wakulima wa Tumbaku,mkuu wa mkoa wa Tabora Ludovick Mwananzila, Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora, Madaktari wa hospitali ya mkoa wa Tabora Kitete, Madaktari wa hospitali ya Rufaa Nkinga, wajumbe wa bodi na watumishi wa WETCU Ltd, Wadau wa Tumbaku, viongozi wa vyama vya siasa na serikali pamoja na Ndugu Jamaa na Marafiki kwa kumuombea, kumpa pole na kumjulia hali.

Ajali hiyo ilitokea majira ya saa moja na nusu usiku siku ya Jumatano ya tarehe 6 mwezi huu katika eneo hilo la Tumbi Manispaa ya Tabora.




No comments: