Na,
Thomas Murugwa, Nzega.
Taasisi
ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU hatimaye imemfikisha mahakamani
muuguzi wa hospitali ya wilaya ya Nzega John David Sambo akituhumiwa kwa
makosa mawili ya kushawishi na kupokea rushwa.
Sambo
alipandishwa kizimbani Ijumaa mbele ya hakimu mkazi mfawidhi wa
wilaya hiyo Seraphine Benard na kusomewa mashitaka hayo na mwanasheria wa TAKUKURU
Edson Mapalala.
Wakili
huyo wa TAKUKURU aliiambia mahakama hiyo kuwa mtuhumiwa huyo alitenda makosa
hayo mawili kati ya Januari 18 na 19 mwaka huu akiwa kwenye kituo chake
cha kazi hospitali ya wilaya ya Nzega.
Mapalala
alidai kuwa tarehe 18 Januari,2016 mtuhumiwa aliomba apewe shilingi laki
moja toka kwa Suleiman Masele ili aweze kumfanyia upasuaji mdogo baba yake
mzazi aitwaye Omary Masele.
Ilidaiwa
katika shitaka la pili kuwa muuguzi huyo akiwa ni mtumishi wa umma alipokea
shilingi elfu themanini toka kwa Suleiman ili kiwe kishawishi cha
kumfanyia upasuaji baba yake mzazi aliyekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa
henia (ngiri).
Mtuhumiwa
alikana makosa hayo na yupo nje kwa dhamana hadi hapo tarehe
5 mwezi huu kesi hiyo itakapotajwa tena ili aweze kusomewa maelezo ya
awali kwa kuwa upelelezi kesi hiyo umekamilika.
No comments:
Post a Comment