Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Tuesday, January 12, 2016

SUMATRA YATANGAZA UTARATIBU MPYA WA KUPATA LESENI



AFISA WA SUMATRA MKOANI TABORA JOSEPH ZOMBWE MICHAEL


Na Paul Christian, Tabora.

Mamlaka ya udhibiti wa usafiri wa nchi kavu na majini SUMATRA mkoani Tabora imetangaza utaratibu mpya wa kutoa leseni kwa wafanyabiashara wa usafirishaji.

Akizungumza na VOT FM STEREO leo asubuhi afisa wa SUMATRA mkoa wa Tabora Joseph Zombwe amesema utaratibu wa sasa unaotumika ni wa kimtandao ambao unahitaji mfanyabiashara kukamilisha taratibu zote muhimu kabla ya kupewa leseni yake.

Amezitaja taratibu hizo kuwa ni pamoja na kulipa kodi za TRA, hati ya malipo ya Bima, hati ya ukaguzi wa polisi,kadi ya gari, leseni ya dereva pamoja na mkataba baina ya mfanyabiashara na dereva husika.

Zombwe amesema utaratibu huo mpya unalengo la kuiongezea serikali mapato, kukwepa kughushi leseni pamoja na kuhakikisha wadau muhimu wanatimiza majukumu yao ipasavyo.

Afisa huyo wa SUMATRA mkoani Tabora amewataka wafanyabiashara wa usafirishaji kutimiza vigezo hivyo mapema kabla ya kufika kuomba leseni  au kuongeza muda wa leseni.
Zombwe amebainisha kuwa utaratibu huo mpya unamruhusu mfanyabiashara kuanza mchakato wa kuomba leseni yake kuongezewa muda mwezi mmoja kabla ya kufikia tarehe ya mwisho.

No comments: