Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Thursday, January 28, 2016

WATU SITA WAKIWEMO WATENDAJI, WALIMU NA MGAMBO WAHUKUMIWA KWENDA JELA KWA RUSHWA, UDANGANYIFU NA KUGHUSHI.




Na,Thomas Katobhaya, Tabora

Watu sita wakiwemo watendaji wa vijiji na walimu wamehukumiwa kutumikia kifungo cha mwaka mmoja jela au kulipa faini ya shilingi laki tano  baada ya kupatikana na hatia ya Rushwa katika kesi mbili tofauti.

Adhabu hiyo imetolewa na hakimu mkazi wa mahakama ya mkoa wa Tabora Jackton Rushwela baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka  ulioongozwa na wakili Edson Mapalala wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU.

Waliopewa adhabu hiyo ni Linso Mohamed ( mtendaji kata ya Ibiri),Sad Mdewa (mtendaji kijiji cha Mkalya), Mapalala Shaban (mtendaji kijiji cha Ibiri) Adam Nassoro (mgambo), Saada Juma Mrisho na Salma Ally Ngozi wote walimu.

Awali Katika kesi ya kwanza iliyokuwa inawakabili maafisa watendaji ilidaiwa  na upande wa mashitaka kuwa walitenda makosa ya kushawishi na kupokea rushwa tarehe 4 Aprili 2012 katika kata ya ibiri wilaya ya Uyui.

Wakili wa TAKUKURU  alidai kuwa siku hiyo mshitakiwa  Mapalala Shabani aliomba rushwa ya shilingi milioni nne toka kwa Rukuba Masalu ili asimchukulie hatua za kisheria kwa kosa la mifugo yake kuharibu mazao.

Katika shitaka la pili lililokuwa linawakabiri washitakiwa wote wanne ilidaiwa na wakili  Edson kuwa walipokea rushwa ya Tsh. milioni 3.2 toka kwa Rukuba.

Hadi mahakama inamaliza shughuli zake ni mshitakiwa mmoja tu kati yao  Said Mdewa ambaye alikuwa ameishalipa faini ya shilingi laki tano  na kuwaacha wenzake wakipelekwa gerezani hadi hapo ndugu zao watakapolipa kiasi hicho cha fedha.

Nao walimu wawili wa shule ya msingi Mabatini ya mjini Tabora waliotiwa hatiani kwa makosa mawili ya kumdanyanya mwajiri pamoja na kughushi walifanikiwa kulipa faini  hivyo kukwepa adhabu ya kifungo cha mwaka mmoja jela.

Awali ilidaiwa na wakili Edson kuwa walitenda makosa hayo  ya kumdanganya mwajiri na kisha kughushi nyaraka wakati wakiwa ni watumishi wa serikali katika idara ya Elimu  mwezi Novemba 2008.

Ilidaiwa kuwa siku hiyo wakiwa ni watumishi walighushi majina kwamba  watu 30 wamehudhuria mafunzo ya siku tano  wakati wakijua kuwa  huo ni uongo kwani mafunzo hayo yalifanyika kwa siku moja.

No comments: