Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Saturday, January 30, 2016

CAMEROON, RWANDA ZATUPWA NJE MICHUANO YA CHAN 2016



CHAN TROPHY
Na Paul Christian.


Timu ya Taifa ya Congo DR imekuwa ya kwanza kufuzu hatua ya nusu fainali ya michuano ya CHAN 2016 inayoendelea nchini Rwanda baada ya kuwaondosha wenyeji Rwanda kwa ushindi wa goli 2 kwa 1 katika mechi ya kwanza ya robo fainali ya Michuano hiyo iliyocheza Jumamosi.

Iliwachukua dakika 11 tu kwa Congo DR kupata bao la kuongoza kupitia kwa Doxa Gikanji aliyeachia shuti kali la mbali na kujaa nyavuni mwa Rwanda.

Licha ya Congo DR kucheza kwa nguvu na kushambulia mara kwa mara lango la wapinzani wao, Rwanda waliweza kuzuia na kulazimisha kipindi cha kwanza kumalizika wakiwa nyuma kwa goli moja.

Kipindi cha pili mashabiki wa Rwanda walilipuka kwa shangwe kufuatia mchezaji Jean-Claude Iranzi kuisawazishia timu yake ya Rwanda na kuifanya kumaliza dakika 90 kwa sare ya 1 kwa 1.

Chui hao wa Congo DR walicheza na kuumiliki mchezo katika kipindi cha pili cha muda wa nyongeza wa dakika 30 na kufanyikiwa kupata goli la pili kupitia kwa Padou Bompunga baada ya walinzi wa Rwanda kufanya makosa.


Mechi ya pili ya robo fainali iliwafanya Ivory Coast kuhitaji muda wa nyongeza baada ya muda wa kawaida wa dakika 90 kumalizika bila kufungana na Cameroon.

Muda huo wa nyongeza wa dakika 30 waliutumia vizuri na kuweza kufunga magoli 3 ya haraka, na hivyo kufuzu hatua ya nusu fainali kwa kuibwaga Cameroon kwa magoli 3 kwa 0.

Mechi zingine za robo fainali zitachezwa leo Jumapili kwa kuzikutanisha
  • Tunisia vs Mali – katika uwanja wa  Nyamirambo,Kigali
  • Zambia vs Guinea – kwenye uwanja wa Umuganda ,Rubavu

No comments: