Na,
Thomas Murugwa, Tabora.
Taasisi
ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU imewafikisha mahakamani watu wawili
kwa tuhuma tofauti mmoja kwa kuhujumu uchumi na mwingine kughushi
nyaraka hivyo wote kusababisha hasara ya mamilioni ya shilingi.
Waliofikishwa
mahakamani ni aliyekuwa afisa misitu msaidizi wa wilaya ya Sikonge
Krety John ambaye anakabiliwa na mashtaka saba ya kutumia madaraka vibaya
na Cathberth Ndogoma aliyekuwa mratibu wa Tabora NGOS Cluster akiwa na tuhuma 19
za kutumia nyaraka kumdanganya mwajiri.
Katika
kesi inayomkabili Krety John ilidaiwa na wakili wa TAKUKURU Edson
Mapalala mbele ya hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Tabora Emanuel
Ngigwana kuwa alitenda makosa hayo kati ya tarehe 26 Machi 2010 na tarehe
25,2012 huko wilaya ya Sikonge na kumsababishia mwajiri hasara ya zaidi ya
shilingi milioni 27.
Wakili
Mapalala aliiambia mahakama hiyo kuwa mtuhumiwa akiwa mtumishi wa Halmashauri
ya wilaya ya Sikonge kama afisa misitu msaidizi alitoa vibali vya kusafirishia
mazao ya misitu kwa watu mbali mbali bila kuzingatia sheria ya misitu.
Wakili
huyo alibainisha kuwa mnamo tarehe 26 Machi 2010 mtuhumiwa kwa makusudi alitoa
kibali chenye thamani ya shilingi milioni tatu na kati ya tarehe 12 Julai na tarehe
16 Oktoba 2010 alitoa vibali vyenye thamani ya shilingi 10,052,800/- bila
kuzingatia sheria ya misitu.
Upande
wa mashitaka ulidai kuwa mtuhumiwa akiwa ni mtumishi wa serikali kati ya
desemba 16/2010 na machi mosi 2012 alitumia madaraka yake vibaya kwa
kutoa vibali vyenye thamani ya shilingi milioni 14,004,000/= na
kuisababishia hasara serikali.
Ilidaiwa
kwenye shitaka la saba kuwa kati ya machi 2010 na machi 2/2012 mtuhumiwa
alishindwa kutimiza majukumu yake na kuisababishia serikali hasara ya
shilingi milioni 27,666,400/=.
Mtuhumiwa
huyo yupo nje kwa dhamana hadi januari 11 mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa.
Katika
kesi inayomkabili Kathberth Ndogoma ilidaiwa na wakili huyo wa TAKUKURU mbele
ya hakimu mkazi wa mahakama ya mkoa wa Tabora Joctan Rushwela kuwa alitenda
makosa hayo kati ya tarehe 11 Novemba 2008 na tarehe 23 Disemba 2008
akiwa mfanyakazi wa taasisi ya Tabora NGOs Cluster.
Wakili
Mapalala alidai kuwa katika kipindi hicho na kwa tarehe tofauti mtuhumiwa kwa
lendo la kudanganya alighushi daftari la mahudhurio likionyesha majina ya
watu walihudhuria mafunzo ya utoaji huduma kwa watu wanaoishi na Virusi vya
Ukimwi na ukimwi majumbani.
Aliongeza
kuwa mtuhumiwa pia alighushi hati mbali mbali za malipo zikionyesha kwamba
amewalipa watu waliohudhuria mafunzo hayo kiasi cha shilingi elfu tano kila
mmoja hivyo kuisababishia hasara Tume ya kudhibiti UKIMWI nchini TACAIDS ambayo
ilitoa fedha hizo.
Mapalala
alidai kuwa mtuhumiwa kwa makusudi alibadili matumizi ya fedha na kusababisha
hasara ya shilingi milioni 6,496,000/- zilizotolewa na TACAIDS
kwa ajili ya mafunzo ya wanaowahudumia wanaoishi na Virusi vya UKIMWI
majumbani .
Mtuhumiwa
alikana tuhuma zote 19 lakini wadhamini wake walishindwa kutimiza masharti ya
dhamana alipelekwa rumande hadi januari 14 mwaka kesi yake itakapoanza usikilizwaji
wa awali.
No comments:
Post a Comment