Na Paul Christian, Tabora
Msanii wa muziki wa kizazi kipya wa mjini Tabora
Manota De Hunter atafanya uzinduzi wa Video yake Mpya inayokwenda kwa jina la “Mkwanja”
kwenye Ukumbi wa buradani wa 101 wa
Mjini hapa.
Akizungumza kwenye kipindi cha Extra Ordinary kilichorushwa
Jumanne na VOT FM STEREO Mwenyekiti wa Tanzanite Entertainment ambaye pia ni
Afisa habari wa Umoja wa Vikundi vya Sanaa Tabora UVISATA Antony Mrope “Mrope
Junior” amesema uzinduzi huo utafanyika tarehe 23 Jan 2016 kuanzia majira ya
saa 2 usiku kwenye ukumbi huo wa 101.
Amesema UVISATA umeamua kumuunga mkono msanii huyo
ili kuonyesha njia kwa wasanii wengine wa fani mbalimbali kuwa umoja huo
unalengo la kuwaleta pamoja wasanii wote ili waweze kujitambua na kuendeleza
vipaji vyao katika sanaa.
Mtunza hazina wa UVISATA Mohamed Ally amesema
uzinduzi huo umepewa jina la “Usiku wa Mkwanja” na kwamba kiingilio kitakuwa
Shilingi 5,000/=
Mohamed ameongeza kuwa usiku huo wa "Mkwanja"
utapambwa na wasanii wengine akiwemo Sultan King, Nassir Wavanilla kutoka
jijini Dar es Salaam pamoja na wasanii wa fani mbalimbali kutoka mkoani Tabora.
No comments:
Post a Comment