Na Paul Christian, Kaliua
Nimetembelea kata ya Kanoge iliyopo Tarafa ya Ulyankulu wilaya ya Kaliua mkoani
Tabora nakutana na mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi wa kata hiyo JOHN
Simon Malela.
Mwenyekiti huyo kwa ujasiri anasema, “wakati
wa kampeni za uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 25 mwaka jana mimi nilikuwa
mkurugenzi wa kampeni katika kata yangu.”
Anasema katika kipindi hicho cha kampeni
alimnadi mgombea udiwani kata ya Kanoge kwa tiketi ya CCM JOHN
Vicent Kahanga, wakati huo huo akimuombea kura mgombea ubunge katika jimbo la
Ulyankulu kwa tiketi ya CCM JOHN Peter Kadutu pia aliwaomba wapiga kura
kumchagua mgombea Urais kwa tiketi ya CCM JOHN Pombe Magufuli.
Mwenyekiti huyo anajivunia tukio la yeye
pamoja na wagombea wa nafasi hizo wakitumia jina moja la JOHN na
kwamba wagombea walishinda katika nafasi zao. CCM OYEEEE!!!!!!!!!
No comments:
Post a Comment