Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Sunday, January 31, 2016

RATIBA YA MECHI ZA LIGI KUU YA UINGEREZA JUMANNE NA JUMATANO



Jumanne 2 Februari, 2016
1.
Norwich City
v
Tottenham
Saa 4:45 usiku
2.
West Ham
v
Aston Villa
Saa 4:45 usiku
3.
Leicester City
v
Liverpool
Saa 4:45 usiku
4.
Asernal
v
Southampton
Saa 4:45 usiku
5.
Sunderland
v
Man City
Saa 4:45 usiku
6.
Man United
v
Stoke City
Saa 5:00 usiku
7.
West Brom
v
Swansea City
Saa 5:00 usiku
8.
Crystal Palace
v
Bournemouth
Saa 5:00 usiku

Jumatano 3 Februari, 2016
1.
Watford
v
Chelsea
Saa 10:45 usiku
2.
Everton
v
Newcastle
Saa 10:45 usiku

MTUMISHI WA AFYA AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA RUSHWA.






Na, Thomas Murugwa, Nzega.

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU hatimaye imemfikisha mahakamani  muuguzi wa hospitali ya wilaya ya Nzega  John David Sambo akituhumiwa kwa makosa mawili ya kushawishi na kupokea  rushwa.

Sambo alipandishwa kizimbani  Ijumaa  mbele ya hakimu mkazi mfawidhi wa wilaya hiyo Seraphine Benard na kusomewa mashitaka hayo na mwanasheria wa TAKUKURU  Edson Mapalala.

 Wakili huyo wa TAKUKURU aliiambia mahakama hiyo kuwa mtuhumiwa huyo alitenda makosa hayo mawili kati ya Januari 18 na  19 mwaka huu akiwa kwenye kituo chake cha kazi hospitali ya wilaya ya Nzega.

Mapalala alidai kuwa tarehe 18 Januari,2016  mtuhumiwa aliomba apewe shilingi laki moja toka kwa Suleiman Masele ili aweze kumfanyia upasuaji mdogo baba yake mzazi aitwaye Omary Masele.

Ilidaiwa katika shitaka la pili kuwa muuguzi huyo akiwa ni mtumishi wa umma alipokea shilingi elfu themanini  toka kwa Suleiman ili kiwe kishawishi cha kumfanyia upasuaji baba yake mzazi  aliyekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa henia (ngiri).

Mtuhumiwa alikana  makosa hayo na yupo nje kwa dhamana   hadi hapo tarehe 5 mwezi huu  kesi hiyo itakapotajwa tena ili aweze kusomewa maelezo ya awali kwa kuwa upelelezi kesi hiyo umekamilika.


POLISI TABORA YAFIKISHA POINTI 24 BAADA YA KUWACHEZESHEA KICHAPO CHA KI-FFU, GEITA GOLD MINE


Na Ramadhan Faraji, Tabora.

Ligi daraja la kwanza imeendelea kushika kasi Jumapili  kufuatia timu ya Polisi Tabora kuikaribisha timu ya Geita Gold Mine kwenye uwanja wa Ally Hassan Mwinyi mjini Tabora.

Mechi hiyo iliyokuwa na ushindani mkubwa iliwasisimua mashabiki wa Polisi Tabora ambao walikuwa na shahuku ya kuiona timu yao ya nyumbani ikifanikiwa kuondoka na pointi 3 muhimu na kujiweka kwenye nafasi nzuri ya kupanda ligi kuu ya Tanzania Bara.

Iliwachukua dakika 81 Polisi Tabora kupitia kwa mchezaji wao Ked Mohamed kuwanyanyua mashabiki wao baada ya kupachika bao la kwanza na la ushindi.

Kwa ushindi huo Polisi Tabora imefikisha pointi 24 sawa na wapinzani wao Geita Gold Mine ambao wanaongoza ligi hiyo wakiwa na pointi 24 na wakiwa na tofauti ya goli moja.

Polisi Tabora ambayo inanyemelea nafasi ya kucheza ligi kuu Tanzania Bara pamoja na wapinzani wao Geita Gold Mine wamebakiza mechi mbili kila timu ili kukamilisha mzunguko wa pili wa ligi daraja la kwanza ambao utaamua timu ipi ipande daraja.

Mwishoni mwa wiki hii Polisi Tabora watawafuata maafande JKT Kanembwa huko Kigoma wakati Geita Gold Mine watawafuata maafande wa JKT Oljoro mjini Arusha.

Tabora Watch inawatakia kila la heri Polisi Tabora kwenye mbio hizo za kupanda daraja.

Wakati huo huo siku ya Jumamosi Rhino Rangers ya Tabora ikiwa kwenye uwanja wa ugenini mjini Musoma ilipoteza mechi yake mbele ya maafande wa Polisi Mara baada ya kukubali kichapo cha bao1 kwa 0 ikiwa ni mwendelezo wa ligi daraja la Kwanza.



MATOKEO YA LA LIGA, CRISTIANO RONALDO AFUNGA HAT-TRICK YA 29



 
CRISTIANO RONALDO AFUNGA HAT -TRICK YA 29
 MATOKEO YA LIGI KUU YA HISPANIA (LA LIGA)

Jumamosi 30 Januari, 2016
1.
Barcelona FC
2-1
Atletico Madrid
2.
Eibar
1-2
Malaga
3.
Getafe
0-1
Athletic Bilbao
4.
Villareal
1-0
Granada
Jumapili 31 Januari,2016
1.
Real Sociedad
2-1
Real Betis
2.
Sevilla
3-1
Levante    
3.
Valencia
0-1
Sporting   
4.
Las Palmas
2-1
Celta Vigo 
5.
Real Madrid
6-0
Espanyol    
Jumatatu 1 Februari,2016
1.
Deportivo
v
Rayo  (22:30)


MSIMAMO WA LA LIGA


Pos
Team
P
W
D
L
GF
GA
GD
Pts
1
Barcelona
21
16
3
2
54
17
37
51
2
Atletico de Madrid
22
15
3
4
31
10
21
48
3
Real Madrid
22
14
5
3
64
20
44
47
4
Villarreal
22
13
5
4
29
18
11
44
5
Sevilla
22
10
6
6
31
23
8
36
6
Athletic Club
22
10
4
8
33
30
3
34
7
Celta de Vigo
22
10
4
8
33
35
-2
34
8
Eibar
22
9
6
7
35
28
7
33
9
Deportivo de La Coruna
21
6
11
4
28
25
3
29
10
Malaga
22
7
6
9
18
20
-2
27
11
Getafe
22
7
5
10
26
32
-6
26
12
Valencia CF
22
5
10
7
26
23
3
25
13
Real Sociedad
22
6
6
10
26
34
-8
24
14
Real Betis
22
5
7
10
15
31
-16
22
15
Espanyol
22
6
4
12
20
41
-21
22
16
Las Palmas
22
5
6
11
23
34
-11
21
17
Sporting de Gijon
21
6
3
12
23
35
-12
21
18
Granada CF
22
5
5
12
24
44
-20
20
19
Rayo Vallecano
21
5
4
12
26
45
-19
19
20
Levante
22
4
5
13
21
41
-20
17