Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Wednesday, December 30, 2015

WATENDAJI WA SERIKALI WATETEE MASLAHI YA NCHI BADALA YA KUMFURAHISHA DKT.MAGUFULI



Bwana Samson Amos akifafanua jambo

 
Na Paul Christian, Tabora.

Viongozi wa serikali wameshauriwa kuwa makini wakati wa kutoa matamko au kuchukua hatua za kiutendaji wakati huu wa kaulimbiu ya hapa kazi tu.

Ushauri huo umetolewa na mshauri wa tiba mbadala wa bidhaa za Tiens mjini Tabora Samson Amosi katika mahojiano maalum na mwandishi wa Tabora Watch Blog.

Amesema kauli ya serikali ya hivi karibuni ya kusitisha matangazo ya wataalam wa tiba mbadala kwenye vyombo vya habari pamoja na kuweka masharti ya kuhariri matangazo hayo kabla ya kwenda hewani inapaswa kutekelezwa kwa umakini ili kutenda haki.

Samson amesema, “kama lengo ni kudhibiti ubora wa bidhaa, huduma au utaalamu wa tiba mbadala itakuwa vyema tukiona juhudi hizo katika matangazo ya vileo, sigara na uzalishaji wa tumbaku bidhaa ambazo zinamadhara ya wazi kwa afya za walaji.”

Amebainisha kuwa baadhi ya bidhaa zinazotumiwa kwenye  tiba mbadala zimetengenezwa kwa virutubisho na madini kama chakula cha ziada kwa watu waliokosa na kusababisha miili yao kushambuliwa na magonjwa mbalimbali.

Samson amesema bidhaa hizo zimetengenezwa baada ya kufanyiwa utafiti wa kina uliothibitisha kufanya kazi kwa ufanisi zaidi kuliko hata dawa zinazotumiwa hospitalini ambazo nyingi zinamadhara kwenye miili licha ya kutibu.

Mshauri huyo wa tiba mbadala amefafanua kuwa  watendaji wa serikali wasitekeleze majukumu yao kwa kumfurahisha Rais John Pombe Magufuli  bali wafanye hivyo kwa kuwa ni wajibu wao wa kulinda na kutetea maslahi ya taifa.

Samson amesema sekta ya afya inahitaji uwekezaji wa maarifa na ufahamu wa hali ya juu katika ugunduzi wa dawa za asili zenye uwezo wa kutibu magonjwa ambayo hayatibiki katika hospitali za mfumo rasmi.

Amefafanua kuwa taifa linapaswa kuwekeza kwenye tafiti zitakazotoa majibu sahihi ya tiba za magonjwa sugu badala ya kubeza na kukumbatia dawa zilizogunduliwa na wataalamu wa mataifa mengine .

Aidha amesema kuwa licha ya kutoa ushauri wa tiba mbadala amekuwa akilipia leseni yake ya biashara shilingi 80,000/= , kodi ya mapato shilingi 200,000/= pamoja na kodi ya pango shilingi 1,200,000/= kwa mwaka hali, inayoonyesha uhalali katika shughuli anazozifanya.

Samson ameongeza kuwa Mamlaka ya Chakula na Dawa TFDA kanda imeagiza kuanza kulipwa shilingi 60,000/= kwa mwaka jambo linaloongeza mzigo mwingine kwa washauri wa tiba mbadala ambao wanatekeleza majukumu yao kwa kamisheni.

Amesisitiza kuwa licha ya Tanzania kuwa na mimea na vitu vingine vya asili wataalamu wake wameshindwa kushirikiana na kugundua dawa, virutubisho au madini kupitia mimea hiyo  kwa lengo la kuzalisha bidhaa za kitanzania  kama zilivyo nchi za Mashariki ya mbali.

No comments: