Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Monday, December 14, 2015

MUSA NTIMIZI:KUTOA MIFUKO 1100 YA SARUJI KWA KATA 11 ZA JIMBO LA IGALULA.



Na Paul Christian, Tabora.

Mbunge wa Jimbo la Igalula wilaya ya Uyui mkoani Tabora ameahidi kutoa mifuko ya saruji 1,100 kwa lengo la kuchochea utekelezaji wa miradi ya ujenzi katika kata 11 za jimbo hilo.

Ahadi hiyo ameitoa Jumatatu alipokuwa akizungumza kwenye kikao alichokipa jina la kamati maalumu kilichohudhuriwa na Madiwani pamoja na  Watendaji wa Kata wa jimbo la Igalula na kufanyika kwenye Ukumbi wa mikutano wa Tabora Rest House mjini Tabora.

Ntimizi amesema mifuko hiyo 1,100 ya saruji ambayo ni mifuko 100 kwa kila kata ameitoa kama kichocheo cha ubunifu na ufanisi wa kutekeleza miradi ya maendeleo ya wananchi kulingana na vipaumbele vya kata husika.

Amebainisha kuwa licha ya kutoa mifuko hiyo 100 kwa kila kata hata sita kuongeza mifuko zaidi ya saruji pale atakapo baini uongozi wa kata husika umesimamia vizuri miradi itakayokuwa imekusudiwa.

Mbunge huyo wa Igalula amewahakikishia wajumbe wa kikao hicho kuwa mifuko hiyo ya Saruji 1,100 ataitoa na kuikabidhi kwao tarehe 10 ya mwezi wa Januari mwaka 2016.

Akizungumzia sekta ya afya amesema lengo lake ni kuhakikisha anaitekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM inayoelekeza kila kijiji kuwa na zahanati na kila kata kuwa na kituo cha afya.

Aidha amebainisha kuwa kutokana na jiografia ya jimbo la Igalula viongozi wa kata wanaowajibu wa kuangalia namna ambavyo kata zinaweza kushirikiana kujenga vituo vya afya kulingana na ukaribu wa kata husika.

Ntimizi amesema atahakikisha anapigania na kutetea maslahi ya watendaji wa vijiji na kata kwa kuwa wanafanya kazi kubwa ya kukusanya mapato ya Halmashauri pamoja na kusimamia miradi ya maendeleo katika maeneo yao.

Amesema watendaji wa kata wanapaswa kuwezeshwa vyombo vya usafiri ili watekeleze majukumu yao kwa ufanisi na kwa viwango vinavyoonekana.
Amesema Kikao hicho alichokiita kamati maalumu kitakuwa kikikutana kila baada ya miezi minne.

Kikao hicho kilihudhuriwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Uyui, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Afisa Mipango wa Halmashauri, wajumbe wa sekretariet ya Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Uyui pamoja na wajumbe wa kamati ya siasa ya CCM  wilayani humo.

No comments: