Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Sunday, December 13, 2015

UMMY:WIZARA ITABORESHA HUDUMA ZA AFYA



Na Catherine Sungura-WAMJW  

Waziri wa Wizara ya afya,maendeleo ya jamii,jinsia,wazee na watoto, Ummy Mwalimu amesema wizara yake itaendelea kusimamia na kuboresha huduma ya afya kwa kuongeza vituo vya kutolea huduma hadi ngazi ya jamii.

Waziri huyo alitoa kauli hiyo Jumamosi wakati akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufanya ziara ya kushtukiza kwenye hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam.

Ummy amesema wizara inatekeleza mpango wa maendeleo ya afya ya msingi(MAMM) ya kujenga zahanati kila kijiji,vituo vya afya kwenye kila kata na hospitali kila wilaya.

Aidha amesema wizara inalojukumu la kusimamia sera  ya afya, wataongeza watumishi wa afya kwa kuongeza udahili wa wanafunzi katika vyuo mbalimbali.

No comments: