Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Friday, December 11, 2015

PADRI ANTONY KATOBA:KANISA KATOLIKI LA BARABARA YA 13 ULYANKULU LIMEJENGWA KWENYE ARDHI YA ILIYOKUWA IKULU YA MTEMI MILAMBO




Na Paul Christian, Ulyankulu.

Paroko wa Parokia ya Kanisa Katoliki Ulyankulu padri Antony Leonard Katoba amesema eneo lilipojengwa Kanisa Katoliki barabara ya 13 Ulyankulu,mkoani Tabora ni la kihistoria kwa kuwa ndipo ilipokuwa Ikulu ya pili ya Mtemi Milambo.

Amesema Ikulu hiyo ya Mtemi Milambo ilijulikana kwa jina la Iselamagazi na ilianza kujengwa mwaka 1879 na kukamilika mwaka 1883.

Padri Katoba anabainisha kuwa Ikulu hiyo ya Iselamagazi ilitumiwa na Mtemi Milambo kiutawala na pia ilikuwa kambi ya jeshi la Mtemi Milambo lililojulikana kama “Walugaluga”.

Aidha Paroko huyo ameeleza kuwa Mtemi Milambo alikuwa na Ikulu nyingine Ikonongo ambapo ndipo yalipokuwa makazi ya Mtemi huyo mashuhuri.

Padri Katoba anasema, “Mtemi Milambo alianza kuijenga Ikulu ya Ikonongo mwaka 1880 na kuikamilisha mwaka 1883.”

Paroko huyo wa Parokia ya Ulyankulu amesema Kanisa Katoliki lilikabidhiwa eneo hilo mwaka 1975 kwa ajili ya kulilinda na kulitunza na kwamba wanaendelea kulitunza na kulienzi.

No comments: