Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Wednesday, December 16, 2015

RHINO RANGERS YAIKWANJUA POLISI TABORA KOMBE LA SHIRIKISHO



 Ramadhan Faraji,Tabora.

Timu ya soka ya maafande wa JWTZ Rhino Rangers ya mjini Tabora Jumanne imewaondoa maafande wa Polisi Tabora kwenye michuano ya kombe la Shirikisho kufuatia ushindi wa mabao 4 kwa 2.

Mechi hiyo iliyozikutanisha timu hizo inajulikana kama Derby ya mji wa Tabora ilichezwa kwenye uwanja wa Ally Hassan Mwinyi na kushuhudiwa na mashabiki wengi.

Iliwachukua dakika 10 za mchezo maafande wa Rhino Rangers kupata bao la kuongoza kupitia kwa mchezaji wake Emmanuel Noel ambapo dakika 5 baadae Polisi Tabora walipata goli la kusawazisha kupitia kwa mchezaji Lucas Patrick.

Timu hizo ambazo zinashiriki ligi daraja la Kwanza nchini zilikamilisha dakika 90 za mchezo zikiwa zimefungana bao 1 kwa 1.

Mwamuzi wa kati Ferdinand Machunde akaamuru kupigwa kwa mikwaju ya penati ili mshindi apatikane na kusonga mbele katika michuano hiyo.

Kwenye upigaji wa mikwaju ya penati Rhino Rangers ilipata penati ya kwanza kupitia kwa Masungu Julias ambapo mpigaji wa Polisi Tabora Michael Chinedu alipoteza mkwaju wake.

Wachezaji wa  Rhino Rangers waliofunga penati zao ni Salum Maji na Imani Mwangasora huku Benedict Solomon akikosa penati yake, kwa upande wa Polisi Tabora aliyefunga penati ya pekee ni Ahamed Mkweche, huku  Mohamed Jimngo na Said Shabani wakipoteza penati zao.

Mwamuzi huyo wa kati Machunde akisaidiwa na Nestory pamoja na Aswire Faresi akamaliza mtanange huo kwa Rhino Rangers kuibuka ushindi wa  jumla ya magoli 4 kwa 2 ya  Polisi Tabora.

No comments: