Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Saturday, December 26, 2015

TABORA NDIO KWETU: WASHEHEREKEA KRIMASI KITETE.



Tabora Ndio Kwetu wakisheherekea Krimasi, Kitete.

Na, Thomas Katobhaya, Tabora.

Wagonjwa wa wodi tano za hospitali ya rufaa ya mkoa wa Tabora Kitete wamesherehekea  sikukuu ya Krismasi pamoja na kikundi  cha wanamtandao kijulikanacho ‘Tabora Ndiyo Kwetu’ kwa kuwapelekea vinywaji, viburudisho, sabuni na mafuta.
 
Kikundi hicho kiliwafariji wagonjwa hao waliolazwa kwenye wodi hizo kwa  kuwapatia vinywaji aina ya juisi, biskuti, sabuni za kufulia na  mafuta ya kupaka.

Mwenyekiti wa Tabora Ndio Kwetu Alexander Ntonge alisema bado wanaendelea kijipanga ili waweze kutoa msaada mkubwa ambao utawanufaisha wagonjwa watarajiwa na wao wakiwemo kwani hakuna binadamu aliye kamilika.

Ntonge alifafanua kuwa wakiwa kama binadamu wanaamini kwamba wagonjwa wanapaswa kusaidiwa kwani baadhi yao upata matatizo wakiwa mbali na ndugu na jamaa zao.
 
Alisema kikundi hicho kilianzishwa  agosti  2014 kikiwa na lengo la kujishughulisha na shughuli za  kijamii  na hadi sasa kina wanachama 90.
Mwenyekiti huyo alisema  mapema mwezi uliopita baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano  wa Tanzania Dkt.John P. Magufuli kuamua  taifa kufanya usafi walimuunga  mkono kwa  kufanya usafi kuelekea siku ya Uhuru Disemba 9,mwaka huu katika hospitali hiyo ya Kitete.

No comments: