Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Thursday, December 17, 2015

IFAHAMU HIFADHI YA TAIFA YA GOMBE, KIGOMA



  Na Paul Christian, Tabora

Hifadhi ya Taifa ya Gombe ni ya pili kwa udogo ikiwa na ukubwa wa kilometa za mraba 56 zilizoambaa sambamba na ziwa Tanganyika, umbali wa kilomita 16 Kaskazini mwa mji wa Kigoma.

Hifadhi hii ni maarufu kwa wanyama adimu Sokwemtu  wanaokaribiana sana na binadamu katika muundo wa “kijenetiki” kwa zaidi ya asilimia 98.
Sokwemtu wanafanana na binadamu kwa muundo wa ubongo na mataya yao.

Hifadhi hii yenye Sokwe waliozoeshwa kwa binadamu imepakana na vijiji vitano vya Mwamgongo, Mtanga,Mgaraganza,Bubango na Chankele.

Hifadhi ya Taifa ya Gombe inakadiriwa kuwa na idadi ya Sokwe 110 ambao wamefanyiwa utafiti tangu mwaka 1960, ikiwa pori la akiba.

Shughuli za utalii katika hifadhi hiyo zilianza rasmi mwaka 1978 baada ya watafiti na uongozi kufanikiwa kuwazoesha Sokwemtu kukaribiana na binadamu.

Gombe ilipandishwa hadhi na kuwa hifadhi ya Taifa mwaka 1968 kutokana na jitihada za Jane Goodall kuanzisha kituo cha utafiti wa Sokwemtu na mazingira yake mwaka 1965.

Utafiti wa tabia za Sokwe tangu mwaka 1960 umekuwa ukifanyika kwa kumfuatilia kila Sokwe tangu kuamka hadi kulala pamoja na kuratibu tabia na matukio yote ya siku.

UJIRANI MWEMA

Kwa mujibu wa taarifa ya Mhifadhi mkuu wa Hifadhi ya Gombe, Noelia Myonga.

Hifadhi ya Taifa ya Gombe imesaidia miradi mbalimbali ya maendeleo katika mkoa wa Kigoma katika kuimarisha ujirani mwema.

Hifadhi imesaidia mradi wa kuimarisha mazingira ya chanzo cha maji cha Mgaraganza, ujenzi wa kituo cha polisi cha mpakani Kagunga na ujenzi wa maktaba ya wilaya ya Kasulu.

Aidha hifadhi imesaidia ujenzi wa bweni la wasichana shule ya sekondari ya Bugamba na vyumba vinne vya madarasa katika shule ya sekondari ya Kagongo.

Hifadhi inatarajia kutekeleza miradi ya ujenzi wa bweni la wasichana shule ya sekondari  Bitale, na uvunaji wa umeme jua kwa vikundi vya uvuvi vya Mwamgongo na Mtanga kwa mwaka 2014/2015.

No comments: