Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Wednesday, December 9, 2015

JE WAJUA: Viongozi mashuhuri wanaong’aa wamezaliwa mwezi wa Oktoba?



Na Paul Christian, Tabora.


Rais wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli ni miongoni mwa Viongozi Mashuhuri waliozaliwa mwezi wa Oktoba, ambapo alizaliwa tarehe 29.10.1959, Rais wa Rwanda Paul Kagame alizaliwa tarehe 23.10.1957, Rais wa Kenya Uhuru M. Kenyatta naye alizaliwa tarehe 26.10.1961.

Rais wa Liberia Ellen Johnson Sirleaf ambaye ni mwanamke wa kwanza barani Afrika kushika wadhifa wa Urais alizaliwa tarehe 29.10.1938 na Rais wa Sierra Leone, Ernest Bai Koroma alizaliwa tarehe 2.10.1953.
             
Viongozi wengine mashuhuri waliozaliwa mwezi wa Oktoba ni pamoja na waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ambaye alizaliwa tarehe 21.10.1949, Waziri mkuu wa Uingereza David Cameroon alizaliwa tarehe 9.10.1966  na Rais wa Urusi Vladimir Putin alizaliwa tarehe 7.10.1952.

Viongozi mashuhuri waliowahi kuongoza nchi mbalimbali na ambao walizaliwa mwezi wa Oktoba ni pamoja na Rais wa awamu ya nne wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete aliyezaliwa tarehe 7.10.1950, Rais wa kwanza wa Kenya  Jomo Kenyatta alizaliwa tarehe 20.10.1891 na Rais Joaquim Chissano wa Msumbiji aliyezaliwa tarehe 22.10.1939. 

Waziri mkuu wa zamani wa Uingereza Margaret Thatcher "iron lady" ambaye anashikilia rekodi ya kushika wadhifa huo kwa muda mrefu zaidi (1979-1990) na akiwa mwanamke pekee kushika wadhifa huo alizaliwa tarehe 13.10.1925.

Viongozi wengine Mashuhuri waliozaliwa mwezi wa Oktoba na kupata kutawala ni pamoja na Rais wa 39 wa Marekani Jimmy Carter aliyezaliwa tarehe 1.10.1924, Rais machachari wa Iran Mahmood Ahmednejad alizaliwa tarehe 28.10.1956 na Mahatma Gandhi kiongozi wa vuguvugu la kudai uhuru na baba wa taifa la India alizaliwa tarehe 2.10.1869.

Watu wengine Mashuhuri waliozaliwa mwezi wa Oktoba ni pamoja na Graca Machel mwanamke aliyewahi kuolewa na Marais wawili kwa nyakati tofauti ambao ni Samora Machel wa Msumbiji na Nelson Mandela wa Afrika Kusini alizaliwa tarehe 17.10.1945 na tajiri maarufu duniani Bill Gates alizaliwa tarehe 28.10.1955.

Wengine ni Roman Abramovich mmliki wa klabu ya Chelsea ya Uingereza alizaliwa tarehe 24.10.1966, mwanasoka mashuhuri wa Agerntina Diego Maradona alizaliwa tarehe 30.10.1960, mcheza soka maarufu wa Brazil Edison Arantes do Nascinanto “PELLE” alizaliwa tarehe 23.10.1940 na mwanamziki mashuhuri wa bongo fleva Diamond alizaliwa tarehe 2.10.1989.

Mchezaji maarufu wa klabu ya Manchester United Wayne Rooney alizaliwa tarehe  24.10.1986.

Watu mashuhuri waliozaliwa mwezi wa Oktoba na nyota zao kung’aa katika chaguzi za kuwania uongozi ni pamoja na Seif Sharrif Hamad katibu mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF na mgombea Urais wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika uchaguzi uliofutwa wa Oktoba 25, 2015 alizaliwa tarehe 22.10.1943.

Katibu mkuu wa zamani wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA aliyegombea Urais wa Tanzania mwaka 2010  Dr. Willbrod P. Slaa  alizaliwa tarehe 29.10.1948 na mke wa Rais wa 42 wa Marekani Hillary Clinton ambaye anawania Urais wa nchi hiyo kwa tiketi ya Chama cha Demokratic alizaliwa tarehe 26.10.1947.

Viongozi mashuhuri waliofariki mwezi wa Oktoba ni pamoja na Rais wa kwanza wa Tanzania Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliyefariki dunia tarehe 14.10.1999,Rais wa kwanza wa Msumbiji Samora Mashel aliyefariki tarehe 19.10.1986 na Rais wa kwanza wa Uganda Milton Obote aliyefariki tarehe 10.10.2005.

No comments: