Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Thursday, December 17, 2015

WAANDISHI WA HABARI MKOANI TABORA WACHEMKA KUNG’AMUA TAFSIRI YA “UNQUALIFIED FINANCIAL AUDIT REPORT”



Na Paul Christian, Tabora.

Waandishi wa habari mkoani Tabora wanaoendelea na mafunzo ya siku tano mjini Tabora juu ya uandishi mahiri wa habari za uchunguzi wamekumbana na changamoto ya kung’amua misamiati inayotumika kwenye taaluma mbalimbali ikiwemo Uhasibu.

Mwezeshaji wa mafunzo hayo Mwandishi Mwandamizi, Fili Karashani aliwataka waandishi hao  kung’amua tafsiri ya misamiati hiyo ya kitaaluma kwa kutoa zoezi la tafsiri sahihi juu ya maneno kadhaa ya kiingereza.

Alisema kila mmoja wenu atafsiri misamiati hii, “Unqualified financial audit report na negative response.”

Msamiati wa Negative response ulipatikana katika sentensi iliyosomeka, “He said, I applied for the job and I got a negative response.”

Lengo la mwezeshaji huyo lilikuwa ni kupima umakini wa waandishi hao wa habari katika kung’amua vitu mbalimbali kwa umahiri na usahihi wakati wa wakufuatilia habari za uchunguzi.

Karashani alitoa majibu ya zoezi hilo kuwa karibu waandishi wote walibaini katika sentensi hiyo ya kiingereza kuwa mkazo uliwekwa kwenye maneno “negative response”.

Aidha Mwezeshaji huyo alitoa zoezi lingine ambalo liliwataka waandishi hao kung’amua tafsiri sahihi ya Kiswahili ya maneno “unqualified financial audit report.”

Baada ya dakika 6 hivi, Karashani alitoa majibu ya zoezi hilo ambayo yalibaini kuwa waandishi wengi walieleza tafsiri ya maneno “unqualified financial audit report” kuwa ni hati isiyoridhisha au chafu inayotolewa na mkaguzi wa mahesabu jambo ambalo halikuwa sahihi.

Mwezeshaji huyo alimtangaza mwenyekiti wa Tabora Press Club Teonest Liwa kuwa mwandishi pekee aliyejibu kwa ufasaha zoezi hilo kwa kutoa tafsiri ya maneno, “unqualified financial audit report” kuwa ni hati safi inayotolewa na mkaguzi wa mahesabu.

Aliongeza kuwa katika uhasibu neno “unqualified” linamaana ya safi au inayoridhisha hivyo ni lazima kuongeza maarifa ya kujua kwa ufasaha misamiati ya kitaaluma ili iwe rahisi kuandika habari za uchunguzi katika kiwango cha uandishi uliotukuka.

Leo waandishi hao wanafanya mazoezi kwa vitendo kwa makundi yaliyopewa majina ya kubuni ya vyombo vya habari ambavyo ni the Mirror,Hapa Kazi Tu,Tabora leo na Kagera Raha.

Mafunzo hayo ya siku tano yalianza siku ya Jumanne na yatakamilika Jumamosi  katika ukumbi wa mikutano wa hosteli ya Moravian mjini Tabora.

No comments: