Na, Murugwa Thomas, Tabora.
Mahakama
Kuu kanda ya Tabora imewataka wananchi wanne waliofungua kesi ya kupinga matokea
ya uchaguzi jimbo la Tabora mjini kulipia shilingi milioni tisa kama dhamana
ndipo shauri hilo liweze kusikilizwa.
Uamuzi
huo umetolewa jana na jaji mfawidhi wa Mahakama Kuu kanda ya Tabora Amir Mruma
baada ya kusikiliza maombi ya wananchama hao wanne wa Chama cha Wananchi CUF
waliowakilishwa na wakili wa kujitegemea Hashim Mziray kutoka jijini Dar es
salaam.
Katika kesi hiyo ya madai na 49/2015 ya
kuomba kupunguziwa gharama ya dhamana ya kupinga matokeo ya uchaguzi mahakama hiyo
imeamuru kila mlalamikiwa alipiwe dhamana ya shilingi milioni tatu.
Jaji
Mruma alisema kuwa katika kesi za uchaguzi sheria inaitaka Mahakama iangalie ni
kiasi gani cha fedha mlalamikaji alipe kama dhamana bila kujali uwezo alionao.
Aliongeza
kuwa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania lilitunga sheria ya gharama za
kesi za uchaguzi kwa lengo la kupunguza kufunguliwa kwa mashauri mengi yasiyo
na msingi.
Jaji
Mruma katika uamUzi wake huo amesema kuwa amepitia maelezo ya pande
zote mbili na kuridhika na upande wa wajibu maombi kuwa walalamikaji wanaouwezo
mkubwa kifedha hivyo wanapaswa kulipa dhamana ya shilingi milioni 15 ili
kesi ya msingi iweze kusikilizwa.
Akifafanua
zaidi jaji huyo alisema kuwa walalamikaj wameshindwa kuleta uthibitisho wa
kuunga mkono maombi yaliyoainishwa katika hati za viapo vyao kwamba
wao ni masikini na kwamba hawataweza kumudu kulipa kiasi hicho cha fedha kama
dhamana.
Awali
upande wa wajibu maombi wakiwakilishwa na wakili Kamaliza Kayaga na Juma
Masanja wakili wa serikali waliiambia mahakama hiyo kuwa waombaji wote wanne
wanapaswa kuleta uthibitisho juu ya kuwa na wategemezi wengi wanaoishi nao.
Naye
wakili Mziray anayewawakilisha walalamikaji ameliambia gazeti hili kuwa
ameridhika na uamzi uliotolewa na kwamba wateja wake watajipanga ndani ya siku
14 waweze kulipa kiasi kilichoamuliwa na Mahakama ili kesi ya msingi iweze
kusikilizwa.
Wanachama
wanne wa CUF Jumanne Mtunda, Johari Kasanga, Shaban Mussa na Thomas Ayengo
wamefungua kesi mahakama kuu kupinga matokeo ya uchaguzi wa jimbo la Tabora
mjini yaliyompa ushindi mgombea wa CCM Emanuel Mwakasaka.
Katika
shauri hilo namba 3/2015 wananchi hao wanadai uchaguzi huo haukuwa wa
huru na wa haki hivyo wanaiomba Mahakama itengue matokeo yake na kumpa ushindi
aliyekuwa mgombea wa Chama Cha Wananchi CUF, Peter Mkufya.
Kwa
mujibu wa sheria ya uchaguzi kifungu na 111 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka
2015 inamtaka mtu yoyote anayefungua kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi alipe
dhamana ya shilingi milioni 15, na
endapo akishindwa fedha hizo zisaidie kulipia gharama alizotumia
mlalamikiwa.
No comments:
Post a Comment