Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Wednesday, December 30, 2015

WATAKAOSHINDWA KUWAPELEKA WATOTO WAO SHULE KUKUTANA NA MKONO WA SHERIA.


Mkuu wa wilaya ya Tabora Suleiman Kumchaya akiwahutubia wakazi wa kijiji cha Kapunze,kata ya Ikomwa

 
Na Paul Christian, Tabora.


Wazazi na walezi wa wilaya ya Tabora wametakiwa kuwapeleka watoto wao shule na endapo watashindwa kufanya hivyo watachukuliwa hatua za kisheria.

Mkuu wa wilaya ya hiyo Suleiman Kumchaya ametoa agizo hilo Jumanne jioni alipokuwa akiwahutubia wakazi wa kijiji cha Kapunze katika kata ya Ikomwa wilayani humo.

Amesema serikali ya awamu ya tano inatoa elimu bure kuanzia darasa la awali hadi kidato cha nne na kwamba wazazi au walezi hawapaswi kuchangia fedha yoyote.

Mkuu huyo wa wilaya ya Tabora amewataka wazazi na walezi wenye watoto wenye umri wa miaka kati ya minne na mitano kuwapeleka kuandikishwa kwa ajili ya kuanza darasa la awali mapema mwaka ujao.

Aidha amesisitiza watoto wenye umri wa miaka sita waandikishwe   darasa la kwanza na kwamba zoezi hilo halipaswi kutozwa fedha.

Kumchaya amesema kwa kuwa jukumu la kutoa elimu bure kuanzia elimu ya awali hadi kidato cha nne liko mikononi mwa serikali hakuna sababu ya mtoto kushindwa kufika shule na kusoma.

Amebainisha kuwa serikali imechukua jukumu la kugharamia madawati, vifaa vya michezo,chakula kwa wanafunzi wa bweni,ujenzi wa miundombinu ya shule ikiwemo vyumba vya madarasa na nyumba za walimu.

Mkuu huyo wa wilaya amesema jukumu la wazazi na walezi ni kuwapatia watoto wao  sare za shule na michezo, vifaa vya kujifunzia kama vile kalamu na madaftari, nauli za kuwasafirisha watoto wao wanapotoka na kurudi shule wakati wa likizo.

Aidha kumchaya ameonya kuwafukuza kazi walimu  watakaobainika kuomba fedha wakati wa kuwaandikisha watoto kujiunga darasa la awali, la kwanza pamoja na kidato cha kwanza.

Ametoa wito kwa wazazi na walezi wilayani humo kutotoa fedha  na endapo watatakiwa kufanya hivyo watoe taarifa ili hatua za kinidhamu zichukuliwe.




No comments: