Na Allan Ntana, Tabora.
WATANZANIA wameaswa kujiepusha na tabia ya uvivu na uzembe ili waingie
mwaka mpya wa 2016 kwa kishindo wakiwa na dhamira ya kufanya kazi kwa bidii ili kujiletea
maendeleo.
Wito huo umetolewa na Askofu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God Mkoa wa Tabora Paul Meivukie katika ibada maalumu ya maadhimisho yasikukuu ya Krismas iliyofanyika usiku wa mkesha wa sikukuu hiyo katika kanisa la Kitete Christian Center mjini Tabora.
Alisema maadhimisho ya sikukuu ya kuzaliwa Yesu Kristu ni fursa pekee kwa kila mwanadamu kuchunguza mienendo yake, tabia, utendaji na uchaji Mungu na kuchukua hatua ya mabadiliko ili kuanza vizuri mwaka mpya.
‘Wito wangu katika krismas hii, tukatae uvivu na uzembe, tudumishe mshikamano wetu na upendano ili mwaka 2016 tuwe na maisha yenye baraka, furaha na amani’, alisema.
Aidha alibainisha kuwa kila mtu anapaswa kuufanya mwaka 2016 kuwa wa kuboresha utumishi wake ili astawi vizuri kiroho na kimwili kwa kuwa aliyezaliwa ni mkombozi, mfalme wa amani na ni mshauri wa
ajabu.
Askofu Meivukie Alinukuu kifungu cha biblia katika kitabu cha Isaya 9: 6 na kusema Yesu alizaliwa ili kuwakomboa wanadamu wote hapa ulimwenguni na wote watakaomsadiki na kuendelea kumtumaini katika maisha yao wataona matendo yake makubwa.
Wito huo umetolewa na Askofu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God Mkoa wa Tabora Paul Meivukie katika ibada maalumu ya maadhimisho yasikukuu ya Krismas iliyofanyika usiku wa mkesha wa sikukuu hiyo katika kanisa la Kitete Christian Center mjini Tabora.
Alisema maadhimisho ya sikukuu ya kuzaliwa Yesu Kristu ni fursa pekee kwa kila mwanadamu kuchunguza mienendo yake, tabia, utendaji na uchaji Mungu na kuchukua hatua ya mabadiliko ili kuanza vizuri mwaka mpya.
‘Wito wangu katika krismas hii, tukatae uvivu na uzembe, tudumishe mshikamano wetu na upendano ili mwaka 2016 tuwe na maisha yenye baraka, furaha na amani’, alisema.
Aidha alibainisha kuwa kila mtu anapaswa kuufanya mwaka 2016 kuwa wa kuboresha utumishi wake ili astawi vizuri kiroho na kimwili kwa kuwa aliyezaliwa ni mkombozi, mfalme wa amani na ni mshauri wa
ajabu.
Askofu Meivukie Alinukuu kifungu cha biblia katika kitabu cha Isaya 9: 6 na kusema Yesu alizaliwa ili kuwakomboa wanadamu wote hapa ulimwenguni na wote watakaomsadiki na kuendelea kumtumaini katika maisha yao wataona matendo yake makubwa.
Mwanadamu ana changamoto nyingi za kiuchumi, kifedha, kimwili na kiroho lakini kuzaliwa kwa Yesu Kristu ni tumaini jipya katika maisha yao kwa kujituma katika kila jambo, yeye ni muweza wakimsadiki atawatoa walipo na kuwapeleka kwenye mafanikio ya kiroho na kimwili katika mwaka 2016, aliongeza.
Aidha aliongeza kuwa aliye na Yesu hatashindwa katika jambo lolote lile kwa kuwa atalindwa na mitego yote ya wabaya, atabarikiwa na kuinuliwa katika maisha yake kiroho na kimwili.
Askofu huyo alisema kuwa Yesu pekee
ndiye anayeweza kubadili huzuni za watu kuwa furaha kama wataendelea kujitoa
zaidi kwake.
Askofu Meivukie alitoa wito kwa Serikali ya awamu ya tano kutunza amani kwa kushughulikia changamoto zilizopo sasa hivi na zinazoendelea kujitokeza ikiwemo suala la uchaguzi wa Zanzibar.
Naye
Mzee wa kanisa hilo Kiongozi Dr Frank Mtimbwa alisema kuzaliwa kwa Yesu Kristu
kunaleta tumaini jipya katika maisha ya kila mwanadamu hivyo aliwataka waumini
hao waendelee kumwamini ili alete mabadiliko katika maisha yao.
Askofu Meivukie alitoa wito kwa Serikali ya awamu ya tano kutunza amani kwa kushughulikia changamoto zilizopo sasa hivi na zinazoendelea kujitokeza ikiwemo suala la uchaguzi wa Zanzibar.
No comments:
Post a Comment