Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Sunday, December 13, 2015

IJUE:HISTORIA FUPI YA MTEMI MILAMBO



Na Paul Christian, Tabora.

Mtemi Milambo alizaliwa mwaka 1820 eneo lililojulikana kwa jina la Ikonongo na alipewa jina la Mbula Kasanda.

Baba yake mzazi na Mtemi Milambo aliitwa Kasanda na mama yake alijulikana kwa jina la Mwasi Mpela.

Babu yake na Mtemi Milambo aliyejulikana kwa jina la Kasele Muhofu na ambaye aliishi miaka 300 baada ya kuzaliwa mwaka 1520 na kufariki mwaka 1820 alimrithisha utemi mjukuu wake Mbula Kasanda (Milambo).

Babu yake Mtemi Milambo, Kasela Muhofu kwa maajabu aliongea akiwa tumboni mwa mama yake kabla ya kuzaliwa na baada ya kuzaliwa hakunyonya maziwa ya mama yake.

Mbula Kasanda (Mtemi Milambo) kabla ya kutawazwa kuwa mtemi alitanguliwa na watemi tisa wa kwanza akiwa Sibuga aliyetawala kuanzia mwaka wa 22BK akafuatiwa na Mkindo wa Kwanza ambaye alirithiwa na Mlowa na kisha kufuatiwa na Moto wa Tatu.

Moto wa Tatu alirithiwa na Nsimba Nchembe ambaye naye alimwachia utawala Kapaya aliyerithiwa na Kasele Muhofu ambaye alimuachia utawala Kasimana Kasele.

Kasimana Kasele alikabidhi utawala kwa Mkindo wa Pili ambaye alimrithisha Mbula Kasanda maarufu kama “Mtemi Milambo.”

Mtemi Milambo alianza kutawala mwaka 1838 katika eneo la Ikonongo huku akiwa na Ikulu mbili za Ikonongo na Iselamagazi.

Kabla ya kifo chake kilichotokana na homa kali, Mtemi Milambo aliacha urithi wa kiti cha utemi kwa mtoto wake wa kike aliyejulikana kwa jina la Kibete mnamo mwaka wa 1884.

Kibete alizaliwa akiwa na ziwa moja yaani "titi moja" la mkono wa kushoto.

Kabla ya Kibete kufariki alikabidhi kiti cha utemi kwa Solomoni Kazwika Milambo ambaye alizaliwa siku ya Jumatatu asubuhi ya tarehe 18 Julai, 1945 ambaye yupo hadi hivi sasa.

Solomoni Kazwika Milambo kabla ya kuzaliwa aliongea akiwa tumboni mwa mama yake na hakunyonya maziwa ya mama yake.


No comments: