Na, Rehema Cleophace,Tabora.
Idadi
ya watu wanaougua ugonjwa wa kifafa na kupelekwa katika hospitali ya rufaa mkoa
wa Tabora Kitete inaendelea kuongezeka kuliko magonjwa mengine ya akili mkoani hapa.
Afisa
muuguzi msaidizi wa magonjwa ya akili katika hospitali ya Kitete bibi Suzan Msagata
amesema idadi ya wagonjwa hao imeongezeka mara mbili kwa mwaka huu kutokana na
upungufu wa dawa za ugonjwa huo unaoikabili hospitali hiyo.
Amesema
hali ya upungufu wa dawa unasababisha idadi ya wagonjwa kuongezeka kutokana na
kutopatiwa matibabu ya kutosha na hali ya kuumwa kujirudia.
Afisa
muuguzi huyo amesema mwaka huu zaidi ya wagonjwa 600 wametibiwa katika
hospitali hiyo na kuruhusiwa na kwamba waliolazwa kwa mwaka huu ni wagonjwa 30.
Akizungumzia
changamoto mbalimbali zinazowakabili katika kitengo hicho cha magonjwa ya akili
bibi Msagata amesema tatizo la kukosekana dawa limekuwa sugu hivyo ameitaka
serikali kuhakikisha inatoa dawa za kutosha ili wagonjwa watibiwe kwa kupewa
dawa za muda mrefu kwa lengo
la kuepuka ugonjwa kujirudia rudia.
Ameitaja
changamoto nyingine kuwa ni jamii kuuhusisha ugonjwa wa kifafa na imani za
kishirikina hali inayosababisha wagonjwa kuongezeka kutokana na wengi wao
kuamini kuwa mgonjwa wao karogwa hivyo kuchukua uamuzi wa kumpeleka kwa mganga
wa kienyeji.
Kutokana
na hali hiyo muuguzi huyo msaidizi amewasihi wananchi kuachana na imani hiyo
badala yake wawapeleke wagonjwa wa kifafa hospitalini
kwa matibabu ambayo hutolewa bure.
No comments:
Post a Comment