Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Wednesday, December 16, 2015

TP MAZEMBE YAANGUKIA PUA KWA MARA NYINGINE HUKO JAPAN



Club America v TP Mazembe
Na Paul Christian, Tabora

Magoli yaliyofungwa kipindi cha kwanza na washambuliaji Dario Benedetto na Martin Zuniga yameiwezesha Timu ya Club America ya nchini Mexico kuibuka na ushindi wa mabao 2 kwa 1 dhidi ya Mabingwa wa Vilabu Barani Afrika TP Mazembe yenye masikani yake Lubumbashi, Congo DR.

Dario Benedetto ndiye aliyekuwa wa kwanza kufumania nyavu za TP Mazembe katika dakika ya 19 ya mchezo baada ya kuunganisha kwa kichwa kross iliyochongwa kutoka winger wa kushoto Paul Aguilar.

Mabingwa wa vilabu barani Afrika TP Mazembe walipata bao lao la kufutia machozi kupitia kwa Rainford Kalaba.

Kocha wa TP Mazembe Patrice Carteron amesema timu yake ilikuwa kwenye kiwango kizuri mwishoni mwa ligi ya mabingwa barani Afrika ingawa walipofika Japan walikuwa na siku tatu za maandalizi kabla ya kucheza mechi yao ya kwanza.

“Tungepata angalau siku 10 zingetosha kutuweka fiti zaidi kiushindani na kutokana na hali hiyo hatukuwa katika hali ya kucheza mechi ya ufunguzi kwa ushindani.”amesema kocha huyo TP Mazembe.

Mechi hiyo ya kusaka nafasi ya tano katika michuano ya Kombe la Dunia kwa ngazi ya mabingwa wa vilabu katika Mabara ilichezwa leo kwenye uwanja wa Osaka Nagai nchini Japan.

Kocha wa Club America iliingia uwanjani akiwa amejeruhiwa baada ya kupoteza mechi ya nusu fainali katika dakika za mwisho za mchezo mbele ya Guangzhou Evergrande wakati kocha wa TP Mazembe Patrice Carteron aliingia uwanjani akiwa na nia ya kuonyesha matumaini baada ya kupoteza mechi yao kwa mabao 3 kwa 0 kutoka kwa Sanfrecce Hiroshima.

Ingawa makocha wote wameshuhudia vijana wao wakicheza mchezo mzuri ni dhahiri kuwa kocha wa Club Americana, Ambriz anakwenda nyumbani akiwa mwenye furaha zaidi.

No comments: